LIVE STREAM ADS

Header Ads

KINANA AZIDI KUISAFISHIA CCM NJIA KATIKA MIKOA YA KANDA YA ZIWA. MAPOKEZI YAKE MWANZA NI NOMA.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Nyehunge wilayani Sengerema katika jimbo la Buchosa,Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza.
Kinana ambaye yupo katika ziara hiyo ameambatana na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, ameanza ziara Mkoani Mwanza baada ya kumaliza ziara katika Mikoa ya Kagera Geita.

Akiwa Mkoani Mwanza atafanya kazi ya kuimarisha uhai wa chama, kusimamia, kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi  ya CCM, pamoja na kusilikiza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
 
  Katibu Mkuu wa CCM ndugu Kinana (kulia) akikagua ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Kata ya Nyehunge Kijiji cha Isaka, Jimbo la Buchosa, wilayani Sengerema, Mwanza jana.
  Katibu Mkuu wa CCM ndugu Kinana  akitoka akikagua ujenzi wa Hospitali ya Wilaya  katika Kata ya Nyehunge Kijiji cha Isaka, Jimbo la Buchosa, wilayaniSengerema, Mwanza jana. 
 Wananchi  wakimshangilia Mbunge wa jimbo la Buchosa,Mh.Charles Tizeba,alipokuwa akizungumza nao kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Ndgugu Kinana kuwasalimia Wananchi  katika Kijiji cha Bupandwa, Jimbo la Buchosa.

  Ndugu Kinana akizungumza na wananchi katika Kijiji cha Bupandwa, Jimbo la Buchosa.
 Ndugu Kinana akifunua kitambaa ikiwa ni ishara ya kuweka jiwe la msingi katika Jengo la Ofisi ya CCM Tawi la Katwe,jimbo la Buchosa wilayani Sengerema mkoani Mwanza.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akipata maelezo mafupi kuhusiana na mradi wa maji katika Kijiji cha Rumeya, Buchosa Wilayani Sengerema.
  Ndugu Kinana akihutubia katika Kijiji cha Nyakarilo, Jimbo la Buchosa, Sengerema.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akiwasalimia wananchi wa kata ya Bukokwa,jimboni Buchosa wilaya ya Sengerema mkaoni Mwanza,pichani kulia ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.
  Kinana akikata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji  katika Kijiji cha Kalebezo, Kata ya Nyehunge, Jimbo la Buchosa.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akimtwisha ndoo ya maji mmoja wa akina mama wa Kijiji cha Kalebezo, Kata ya Nyehunge, Buchosa baada ya kuzindua mradi wa maji.
 Mbunge wa Jimbo la Buchosa, Charles Tizeba akimtwisha ndoo ya maji mmoja wa akina mama wa Kijiji cha Kalebezo, Kata ya Nyehunge, Buchosa baada ya kuzindua mradi wa maji.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara iliofanyika kwenye kijiji cha Nyehunge jimbo la Buchosa.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza mmoja wa wakazi wa kijiji cha Nyehunge wilayani Sengerema katika jimbo la Buchosa,alipokuwa akiuliza swali .
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akilakiwa kwa
furaha na Mbunge wa Jimbo la  Sengerema, ambaye pia ni mmoja wa wana CCM waliochukua fomu ya kuomba kuwania urais ndani ya chama hicho, William Ngeleja alipowasili katika Kata ya Nyamadoke, Jimbo la Buchosa,, wilayani Sengerema, kuanza ziara rasmi katika majimbo yote ya Mkoa wa Mwanza jana.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la  Sengerema, ambaye pia ni mmoja wa wana CCM waliochukua fomu ya kuomba kuwanua urais ndani ya chama hicho, William Ngeleja, alipowasili wilayani Sengerema.
Picha:Jiachie Blog

No comments:

Powered by Blogger.