TANZANIA BADO INATAFUNWA NA UINGIZAJI, USAFIRISHAJI NA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA.
Katikati
ni Edwin Soko ambae ni Mwenyekiti wa OJADACT akitoa taarifa kwa Vyombo vya
Habari jana juu ya Maadhimisho ya Siku ya Kupiga Vita Matumizi ya Dawa za
Kulevya Duniani yanayotarajiwa kufanyika Kesho. Kulia ni Neema Joseph ambae ni
Mhasibu wa OJADACT na Kushoto ni Isaack Wakuganda ambae ni Afisa Jinsi OJADACT.
Na:George GB Pazzo
Wakati
Tanzania leo ikiungana na Mataifa mbalimbali duniani Kuadhimisha Siku ya Kupiga
Vita Matumizi ya dawa za Kulevya, imeelezwa kuwa bado Uingizaji, Usafirishaji
na matumizi ya dawa hizo yako katika kiwango cha hali ya juu hapa nchini.
Hayo
yalielezwa hii jana na Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari wa kupiga
vita matumizi ya dawa za Kulevya na Uharifu nchini OJADACT Edwin Soko, wakati
akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusiana na Maadhimisho hayo.
Soko
alibainisha kuwa ripoti zinaeleza kwamba Tanzania ni kinara wa kupitisha dawa
za kulevya katika nchi za afrika mashariki huku akibainisha kuwa katika Mkoa wa
Tanga pekee katika kipindi cha kuanzia mwaka 2010 hadi mwaka huu, ukamataji wa
dawa za kulevya za aina mbalimbali uliongezeka kutoka kilo 145 hadi kilo 813.
Aidha
Soko alibainisha kuwa Kumekuwa na uzembe wa
makusudi kutokana na Serikali kushindwa kutaja nafasi ya Nchi kimataifa juu ya tatizo la dawa za kulevya na badala yake imekuwa ikificha uhalisia wa tatizo hilo ambalo amesema kuwa limekuwa kikwazo katika
jamii kwani takwimu zinaonyesha kuwa katika Mkoa wa Mwanza pekee kuna zaidi
ya Watumiaji wa dawa za kulevya za aina mbalimbali wapatao elfu Kumi ambapo Wilaya za Nyamagana na Ilemela
zina watumiaji zadi ya Elfu tatu Mia tatu.
Kutokana
na hali hiyo Soko alisema kuwa OJADACT inatoa rai kwa Serikali kwamba Vita dhidi
ya dawa za kulevya
zinahitaji nguvu za pamoja ili
kukomesha biashara hiyo pamoja na
Serikali na taasisi mbalimbali kujikita katika kutoa
elimu ya kutosha
juu ya dawa za kulevya.
Aliongeza
kuwa Upatikanaji wa sera
ya dawa za kulevya
uharakishwe ili kusaidia
kumaliza tatizo hilo pamoja na
kuhakikisha kuwa Sheria mpya ya
dawa za kulevya ya mwaka 2014 inasimamiwa na kutekelezwa ipasavyo ili kuleta tija kwa Taifa.
Mbali
na hayo Soko alisema kuwa Vita
dhidi ya dawa za kulevya inapaswa kutangazwa kuwa ni janga la kitaifa huku akisisitiza kuwa moja ya
sifa za Rais wa Tanzania ajaye iwe ni kuwa na
uwezo wa kukabiliana na biashara
ya dawa za kulevya kama
alivyofanya Rais Richard
Nickson wa Marekani.
Kitaifa Maadhimisho
hayo yanafanyika katika Wilaya Bagamoyo Mkoani Pwani ambapo katika
Mkoa wa Mwanza yanafanyika Katika Kata ya Igogo Wilayani
Nyamagana ambapo yanaambatana na Kaulimbiu isemayo "Jenga Jamii, Maisha na
Utu bila Dawa za Kulevya".
No comments: