ZAIDI YA WAENDESHA BODABODA 200 WAUAWA MKOANI MWANZA HUKU BODABODA ZAIDI YA 3,000 ZIKIPORWA.
Na:George GB Pazzo
Waendesha Pikipiki maarufu kwa Jina la bodaboda zaidi ya 200 wameuawawa Mkoani Mwanza kutokana na matukio ya kuvamiwa na kutekwa huku pikipiki zaidi ya 3,000 zikiibiwa.
Waendesha Pikipiki maarufu kwa Jina la bodaboda zaidi ya 200 wameuawawa Mkoani Mwanza kutokana na matukio ya kuvamiwa na kutekwa huku pikipiki zaidi ya 3,000 zikiibiwa.
Hayo
yalielezwa wiki iliyopita na Katibu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza Abubakary Hussein,
alipokuwa akizungumza na Mtaa kwa Mtaa ya Radio Metro Fm katika Ofisi za Umoja
huo zilizopo Kata ya Mbugani Jijini Mwanza.
Hussein
alisema kuwa idadi hiyo ni kwa kipindi cha kuanzia Mwaka 2011 hadi mwa mwaka
huu, idadi ambayo amebainisha kuwa inawatia hofu kubwa waendesha pikipiki katika
shughuli zao.
Hussein
alibainisha kuwa asilimia kuwa matukio hayo hutokea kwa Waendesha pikipiki
kukodishwa na baadhi ya waharifu ambao hujifanya ni abiria na kisha kuwateka na
kuwapora pikipiki jambo ambalo wakati mwingine husababisha umauti kwa waendesha
pikipiki.
Katika hatua
nyingine Hussein aliziomba halmashauri za Mkoa wa Mwanza ikiwemo Hamashauri ya
Jiji la Mwanza kuainisha vituo vya Waendesha pikipiki kwa lengo la kusaidia
kuwatambua waendesha pikipiki.
Makamu
Mwenyekiti wa Umoja huo wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza Seif Mussa Kagoma
alibainisha kuwa kwa muda mrefu wamekuwa na juhudi za kutaka kuubaini mtandao
wa Wezi wa Pikipiki Mkoani Mwanza, lakini juhudi hizo zimekuwa zikikwamishwa na
baadhi ya polisi ambao wamekuwa wakirudisha nyumba jitihada za kubaini mtandao
huo.
Alisema kuna
mtuhumiwa wa wizi wa pikipiki aliwahi kukamatwa Mkoani Mwanza na akaahidi
kuwataja wenzake baada ya kufikishwa katika kituo cha Polisi, lakini mtuhumiwa
huo ilielezwa kuwa alifikishwa Mahakamani kabla hata hajawataja wenzake jambo
ambalo linakwamisha kuubaini Mtandao wa wezi wa Pikipiki Mkoani Mwanza.
Juhudi za kupata idadi ya Waendesha Bodaboda waliouawa na Bodaboda zilizoporwa katika kipindi cha mwaka 2011/15 pamoja na juhudi za kukabiliana na matukio hayo kutoka jeshi la polisi Mkoani Mwanza bado zinaendelea.
Credit.Radio Metro
Credit.Radio Metro
No comments: