LIVE STREAM ADS

Header Ads

SEHEMU YA NNE: JIFANYIE UCHUNGUZI KATIKA MAMBO YAFUATAYO MAISHANI MWAKO.

HUMPHREY MAKUNDI (KULIA) NA

ALLARD MINJA (KUSHOTO), WOTE WANATOKA LIFE SECRETS COMPANY MWANZA.


4.TISHIO NI NINI
Nipo na kamusi yangu ninayoipenda ya webster naangalia maana ya tishio(threat) na inasema; Ni mtu au kitu ambacho kinaweza kuleta shida au madhara.

Sasa usichanganye maneno haya mawili tishio(threats) na vizuizi(restrictions) maana vizuizi ni kitu kingine kabisa ambacho kinamaanisha sheria au utawala ambao unazuia au kuthibiti kitu.

Katika maisha yetu ya kila siku kuna baadhi ya vitu ambavyo tukiwa na tabia ya kuvifanya huwa vinazuia uwezekano wa kupata kile ambacho tunakihitaji kukipata kwa kiasi kikubwa na hivi vitu ndivyo vinaitwa tishio au kiingereza threats.

Tishio katika maisha yako wewe ni nini, je ni pombe ambazo umekuwa unakunywa kila kukicha na ukajikuta unakojoa mabati, mifuko ya theluji na misumari kila siku? au labda wewe mzuri sana katika kupoteza muda kwa mambo yasio na maana, au labda wewe ni bingwa wa kuvuta sigara na unajifanya huoni lile onyo la uvutaji sigara ni hatari kwa afya yako au pengine wewe ni bigwa wa kuvuna vitu ambavyo haujavipanda(mwizi), tambua siku wakikushika watakuchoma moto.

Mimi tishio katika maisha yangu lilikuwa kuangalia movie na siries, nafurahi sana siku hizi sijui siries au muvi ni nini na nilikuwa nikipoteza muda mwingi sana kwenye kuangalia hivi vitu ambavyo kimsingi sijawahi kuona faida yake kwangu ukilinganisha na muda niliokuwa napoteza kuangalia.

Kuna kitu kinaitwa utumwa, unajua mtu kuwa mtumwa sio mpaka avalishwe sare na afungwe gerezani. Unaweza ukawa mtumwa ukiwa huru, mfano kama wewe unapoteza zaidi ya masaa mawili kila siku kuangalia box lenye pembe nne (Tv)wewe ni mtumwa na unatakiwa kutafuta namna ya kujikomboa kutoka katika utumwa huo.

Hebu fanya hesabu rahisi kabisa kwa watu 100 wanaopoteza muda wa masaa masaa kuangalia lile box (Tv, Movie,series) tena kwa vitu visivyowajenga kila siku, kumbuka wanafanya hivi muda ambao miili yao bado ina nguvu na ingeweza kufanya kazi lakini wanaamua tu kuangalia lile box na kupoteza muda.

Angalia watu 100 wanaopoteza muda pasipo sababu za msingi, Ngoja nichukue kikokotoleo changu, niweze kupiga mahesabu kwa watu 100 Tu ambao wanapoteza muda wa saa nne kuangalia Tv hawafanyi kazi yoyote ya msingi na ni vijana wenye nguvu na afya tele.

Ngoja nikuonyeshe wanarudisha taifa nyuma kiasi gani,
100x4=400 watu 100 wanapoteza kila siku masaa 400 hii ikiwa inamaanisha kama wangefanya kazi, taifa lingepata masaa 400 ya ziada ila wanayapoteza maadamu wanaangalia box.

Nagawanya hapa kwa 24 ili nipate siku, 400/24=16.66 tufanye siku 16
Kwa hivyo hawa watu 100 wanaoangalia Tv masaa 4 kila siku wanarudisha taifa nusu mwezi kila siku maana hawafanyi kazi ipasavyo.

Sasa fikiria watu 1000 inakuwa vipi je watu 10,000 je watu 100,000 ambao hawafanyi kazi wanaangalia Tv tu, taifa linarudi nyuma kiasi gani.

Kwa hesabu la haraka kama ningeendelea na kikokotoleo changu ina maana kama watu 100 wanapoteza nusu mwezi kila siku kwa kuangalia tv masaa manne, Ina maana kwa mwaka wangepoteza miezi 6 hivyo watu hawa 100 wanaopoteza muda wanarudisha taifa nyuma miezi sita kila mwaka.

Sasa piga mahesabu ya watu 1000, 10000, 100000, Milioni na kadhalika uone balaa lake. Eeeeeeh ndio nakuonesha namna unavyopoteza muda ni lazima utumie muda wako vizuri mafanikio yamefichwa katika muda kila mtu ana masaa 24 tofauti ipo kwenye namna gani unatumia mda wako.

Hebu tuangalie tishio lingine la madawa ya kulevya. Mtakuwa mashahidi wazuri kwamba wanamuziki wengi na vijana wa hapa nchini kwetu wamekuwa wakipatwa na tishio moja kubwa ambalo ni kutumia dawa za kulevya kitendo, hiki kimekuwa kikisababisha madhara katika afya zao, miili yao,familia zao,jamaa na rafiki zao na nchi kwa ujumla maana nchi yetu imekubwa na kashfa mbaya,na hii inachafua sifa ya nchi yetu.

Hebu kaa chini tafakari ni watu wangapi leo hii wamepoteza maisha yao kwa kutumia dawa za kulevya?

Na je ni mzigo mkubwa kiasi gani wamekuwa wakitwika familia zao ? haya ni maswali magumu kuyameza na tunahitaji Kumwomba Mungu atuokoe katika hili janga na kwa kiasi kikubwa vijana ndio wamekuwa wakiathirika na haya madawa, hii ni hatari maana vijana ndio nguvu kazi ya taifa.

Tofauti kubwa kati ya vijana na wazee ni kwamba vijana wanaweza wakatumia akili pamoja na nguvu kwa wakati mmoja lakini wazee ni akili tu nguvu hawana.

Hebu jifunze namna ya kuepukana na hilo Tishio ambalo ndio linasababisha wewe kutokuendelea katika maisha yako, kumbuka kila kitu kinaweza kikabadilika kama kweli ukiamua kujifunza na ukanuia kwamba unataka madadiliko.

Vijana wenzangu tuamke na tufanye kazi kwa akili na nguvu zetu, achana na mambo ya vijiweni, piga kazi na jifunze kila siku, tembea na waliofanikiwa na lazima nawe utafanikiwa.
Itaendelea...
IMEANDALIWA NA LIFE SECRETS COMPANY YA JIJINI MWANZA AMBAO NI WATAALAMU WA AFYA NA MAENDELEO BINAFSI.
Email: allnhumph@gmail.com Phone: 0689 45 26 70/0765 53 68 42

Soma HAPA Sehemu ya Tatu

No comments:

Powered by Blogger.