KESI YA MAUAJI INAYOMKABIRI MKURUGENZI WA MABASI YA J4 YATAJWA. SOMA MAAMUZI YAKE.
Waandishi wa Habari Jijini Mwanza wakiwajibika Mahakamani.
Na:Binagi Media Group
Kesi ya Mauaji inayomkabiri Mkurugenzi wa
Mabasi ya J4 yanayofanya Safari zake katika Mikoa ya Mwanza na Mara Juma
Mahende mwenye umri wa miaka 45, kwa mara ya tatu hii leo imetajwa tena katika
Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Kanda ya Mwanza.
Mahende anakabiliwa na kesi ya kutumia
bastola kutekeleza mauaji ya watu wawili Jijini Mwanza ambao ni Ally Mohamed
mwenye umri wa miaka 35 mkazi wa Igoma na Cloud Steven mwenye umri wa miaka 39
mkazi wa Nyasaka baada ya kutokea marumbano miongoni mwao julai 14 mwaka huu majira
ya saa usiku katika eneo la Buzuruga.
Mwendesha Mashtaka wa Serikali Subira
Mwandama aliiambia Mahakama kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado unaendelea na
utawasilishwa pindi utakapokamilika.
Hakimu Mfawidhi Mkoa wa Mwanza Wilbert
Chuma aliiahirisha kesi hiyo hadi tarehe 27 mwezi huu itakapotajwa tena ambapo
mtuhumiwa huyo amerejeshwa rumande.
No comments: