KESI YA MAUAJI INAYOMKABIRI MKURUGENZI WA MABASI YA J4 YAENDELEA KUUNGURUMA JIJINI MWANZA.
Na:Binagi Media Group
Kesi ya Mauaji inayomkabiri Mkurugenzi wa Mabasi
ya J4 yanayofanya Safari zake katika Mikoa ya Mwanza na Mara Juma Mahende
mwenye umri wa miaka 45, leo imetajwa tena katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa
wa Mwanza.
Mahende amefikishwa Mahakamani hapo ikiwa ni
mara ya nne na tuhuma zinazomkabiri za kutumia bastola kutekeleza mauaji ya
watu wawili Jijini Mwanza ambao ni Ally Mohamed mwenye umri wa miaka 35 mkazi
wa Igoma na Cloud Steven mwenye umri wa miaka 39 mkazi wa Nyasaka yaliyotokea
mwao julai 14 mwaka huu majira ya saa usiku katika eneo la Buzuruga baada ya
kutokea marumbano miongoni mwao.
Mwendesha Mashtaka wa Serikali Judith Nyaki
ameiambia Mahakama kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado unaendelea na kwamba utawasilishwa
Mahakamani hapo pindi utakapokamilika.
Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza Bahati Chitepo
ameahirisha kesi hiyo hadi Septemba tisa mwaka huu itakapotajwa tena ambapo mtuhumiwa huyo
amerejeshwa rumande.
Mahende alifikishwa Mahakamani hapo ikiwa ni
mara ya nne na kusomewa mashtaka ya kutumia bastola kutekeleza mauaji ya watu
wawili Jijini Mwanza ambao ni Ally Mohamed mwenye umri wa miaka 35 mkazi wa
Igoma na Cloud Steven mwenye umri wa miaka 39 mkazi wa Nyasaka yaliyotokea mwao
julai 14 mwaka huu majira ya saa usiku katika eneo la Buzuruga baada ya kutokea
marumbano miongoni mwao.
Mwendesha Mashtaka wa Serikali Judith Nyaki
aliiambia Mahakama kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado unaendelea na kwamba utawasilishwa
Mahakamani hapo pindi utakapokamilika.
Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza Bahati Chitepo aliahirisha
kesi hiyo hadi Septemba tisa mwaka huu
itakapotajwa tena ambapo mtuhumiwa huyo amerejeshwa rumande.
No comments: