LIVE STREAM ADS

Header Ads

SEHEMU YA PILI: UGONJWA WA KISUKARI UNAVYOATHIRI JAMII.

Soma HAPA Sehemu ya Kwanza Ili Twende Sawa.
Kundi la pili ni wagonjwa ni ambao kongosho lao haliwezi kutoa kichocheo cha Insulini kabisa. Hwa ni lazima watumie tiba na dawa(sindano za Insulin) ili kuwezesha sukari inayopatikana kwenye damu kuingia katika viungo vya mwili kama ini na misuli, hivyo wanatakiwa kuchoma sindano kabla ya kula kulingana na aina ya insulini aliyonayo mgonjwa.

Pia anasema dawa ya Insulini imegawanyika katika makundi matatu ambayo ni ;
Insulini  ya maji yenye ufito wa rangi ya njano,ambayo inaanza kufanya kazi baada ya dakika 30,na inadumu kwa masaa 4 hadi 6.

Insulini ya maziwa yenye ufito wa rangi ya kijani hufanya kazi baada ya masaa 2,inadumu kwa muda wa masaa12 hadi 16.

Insulini ya mchanganyiko yenye ufito wa rangi ya brauni,hufanya kazi baada yadakika 30,inadumu kwa masaa 12 hadi 16.

Pia sindano hizo uchomwa sehemu  za bega ,tumbo,makalio, begani a tumbo ni pale unapochomwa na mtu,  dawa hizo zinatakiwa kuhifadhiwa  katika jokofu,mtungi au kopo la mkaa.

Anasema viashiria vinavyoweza kupelekea kuugua  ugonjwa wa Kisukari ni kiriba tumbo,unene uliopitiliza, historia ya kisukari kwenye ukoo,baadhi ya madawa yanasababishaugonjwa huo,msongo wa mawazo, umri zaidi ya miaka 40, kutojishughulisha, kutokufanya mazoezi ipasavyo.

Pia wakinanamama wanajifungua watoto wenye uzito mkubwa zaidi ya  kilo 4,maradhi yatokanayo na kuharibika kongosho,tezi ya shingo,wakina mama wenye historia ya kuwa na kisukari wakati wa ujauzito,wako katika kundi hatarishi la kupata kisukari hapo baadae pamoja na watumiaji wa pombe na sigara.

Mhana anazitaja dalili za mtu kujua kuwa ana ugonjwa wa Kisukari kuwa ni pamoja na;
Kiu ya mara kwa mara na unywaji wa maji mengi ata kama ni wakati wa baridi,kukojoa mara kwa mara mkojo mwingi,kupungua uzito bila ya sababu maalumu ata kama unakula vizuri, kizunguzungu, kutoona vizuri au kupungua kwa uwezo wa kuona.

Nakauongeza kuwa dalili za sukari kupungua mwili kwa mtu ambaye nimuathirika wa ugonjwa wa kisukari tayari ni,kumwa na njaa sana,kuwa na hasira ata kwa kitu kisichoeleweka,mwili kukosa nguvu,kupungua uwezo wa kufikiri,jasho jembamba,mapigo ya moyo  kwenda haraka haraka,kuumwa kichwa ,kutetemeka,na kichefuchefu.

Na kwa baadae kama hajapatiwa tiba mapema atatokwa na jasho jingina mwili kuwa wa baridi,kupelekea hadi kupoteza fahamu,degedege na wakati mwingine kufunga kauli au kupoteza maisha.

Pia Mhana anaelezea madharayatokanayo na ugonjwa wa kisukari kuwa ni pamoja na kupatwa na kiharusi, kupooza na kupoteza fahamu(kumbukumbu), upungufu wa kuona ,mtoto wa jicho,magonjwa ya kinywa na kung’oka meno,shinikizo la damu,mshtuko wa moyo na kushindwa kufanya kazi,kupungua kwa nguvu za kiume hatimaye kukosa kabisa,ganzi katika mwilividonda na hatimaye kukatwa viungo vya mwili hasa miguu na vidple vyake.

Anaelezea mambo 5 ambayo mgonjwa wa kisukari anatakiwa kuzingatia na kuyafuata ili kumfanya aishi maisha marefu.

Mosi ni Usafi wa Kinywa na Meno;mgonjwa wa kisukari anatakiwa kupiga mswaki angalau mara Mbili ni kwa siku,ikibidi kila baada ya mloili kuondoa mabaki ya chakula kinywani yanayoweza kusababisha kutengeneza bacteria watakaoshambulia kinywa.

Tatu ni Kutumia mswaki bora,ili kuepuka madhara yatokanayo na michubuko kwenye fizi.Dawa ya meno ni nzuri lakini inapokosekana basi mgonjwa anashauriwa kutumia jivu la mkaa au chumvi.


Nne Mgonjwa wa kisukari anashauriwa kumuona daktari au wataalamu wa magonjwa ya kinywa na meno angalau mara moja kwa mwaka kwa wale wasiokuwa na tatizo, ila kwa wenye matatizo ya fizi na kutoboka kwa meno wamuone daktali mara 1hadi 3 kwa mwaka kulingana na uwezo wa mtu.

Na tano ni Utunzaji wa miguu ambapo ugonjwa wa kisukari huleta madhara ya miguu kwa kuathiri mishipa ya fahamu na mzunguko wa damu,matokeo yake mgonjwa huanza kuhisi ganzi,hivyo anatakiwa kutunza miguu ili kupunguza ukatwaji viungo hasa miguu.

Hata hivyo mgonjwa anapaswa kuhakikisha kuwa miguu yake anaisfisha vizuri kisha kuikausha mara baada ya kusafisha kwa kutumia taulo au kitaambaalaini na safihasa katikati ya vidole ,pia anapaswa kuikagua kila mara/siku.

Apake mafuta ili kuzuia mipasuko ya ngozi, kama ni mnene sana hawezi kuinama, inatakiwa aombe msaada wa ndugu aliye karibu, pia anatakiwa kuvaa viatu muda wote ndani na nje ya nyumba ili kuepusha kuchomwa na vitu vyenye ncha kali na kusababisha kidonda ambacho ni Atari kwa mwili wake.

Pia anapaswa kusafisha mwili mara kwa mara,pia awe na uwezo wa kugundua tatizo mapema katiksa mguu wake kama kidonda ,lengelenge,kubadilika kwa rangi kwenye mguu uvimbe au mchubuko wowote,ili akapatiwe matibabu haraka kabla ya tatizo kuwa kubwa.

Utunzaji wa kucha; Mgonjwa wa kisukari anatakiwa asiwe na kucha ndefu,kwani anaweza kujichubua nazo wakati wa kutembea au vinginevyo na kusababisha kidonda ambacho kitapelekea kukatwa kwa viungo  mwili kama mguu.

Itaendelea, Imeandaliwa na Judith Ferdinand; 0757804962 Kwa msaada wa mtandao na mashirika ya habari.

No comments:

Powered by Blogger.