LIVE STREAM ADS

Header Ads

SEHEMU YA TATU: UGONJWA WA KISUKARI UNAVYOATHIRI JAMII.

Soma HAPA Sehemu ya Pili ili Twende Sawa.
Mgonjwa pia anatakiwa atumie kitu kisichokuwa na ncha kali mfano mashine ya kukatia kucha,na kama anatatizo la kutoona hapatiwe msaada.
Pia akate kucha kwa kufata mzunguko ili asije kuacha ncha ,ambayu inaweza kumchoma au kumkata na kumsababishia kidonda.
Uvaaji wa viatu; Mgonjwa wa kisukari anatakiwa kuzingatia kuvaa viatu muda wote,pia kutovaa viatu na soksi zinazo bana ili kuepuka kuathiri mzunguko wa damu,mishipa ya fahamu,michubuko ya ngozi,malengelenge  na hatimaye kusababisha vidonda.
Pia mgonjwa anatakiwa kuchunguza viatu kabla ya kuvaa ,ili kujua kama kuna msumari au wadudu watakaoweza kusababisha kumdhru na kupelekea kupata kidonda.
Viatu ndani viwe vilaini na kwenye kisigino nje vigumu ili kusaidia kuzuia vitu vyenye ncha kali kama msumari,vipande vya chupa kutomdhuru vilevile view vyenye visigino vifupi.
Moto; mgonjwa wa kisukari anatakiwa kutopenda kuota moto,naikitokea ameota anatakiwa kuchukuliwa tahadhari ili asiweze kuungua na kusababisha jeraha ambalo ni hatari kutokana na hali yake.
Wakati wa kupika anatakiwa asitumie kitaambaa kushikia sufuria au chungu na badala yake atumie mbanio,baada ya kupika ni vyema kuzima moto kwa maji ya baridi,ili kuepuka kukanyaga na kuungua.
Pia kama anatumia maji ya moto kuoga inabidi atumie kiwiko kupima kama yanafaa ili kuepuka mchubuko.
Mhana anaeleza kuwa mgonjwa wakisukari anatakiwa kula chakula kwa kuzingaria mlo kamili ambao unamakundi matano ya chakula kama.
Kundi la kwanza  la Vyakula vya nafaka, mzizi na ndizi, mgonjwa anatakiwa kutumia aina ya chakula hiki kwa kiwango kidogo, ambacho ni sawa na ngumi yake, ila visiwe vimekobolewa.
“Vyakula vya nafaka ni kama mahindi, ngano, mchele, ulezi, mtama, uwele. Vyakula vya mzizi viazi mviringo, magimbi, viazi vikuu, mihogo, viazi vitamu.
Aina ya ndizi zote,lakini mgonjwa anapaswa kula kiasi ili asisababishe,kushiba sana na kupelekea sukari kupanda”. Anasema Mhana.
Kundi la pili ni vyakula jamii ya kunde na asili ya wanyama; Anasema jamii ya kunde ni maharage, kunde, njugumawe, mbaazi, njegere, choroko, karanga, dengu na fiwi, nazinatakiwa kula kiasi chja ngumi.
Vyakula vyenye asili ya wanyama ni aina zote za nyamaambayo mgon jwa anapaswa kula nusu kilo kwa wiki,maziwa kunywa kila siku nusu lita, samaki, jibini, dagaa, mayai matatu kwa wiki, pamoja na wadudu wanaoliwa kama kumbikumbi na senene.
Kundi la tatu ni mbogamboga; Hizi hujumuisha zile za majani yanayoliwa kama majani ya maboga, kunde, maharage, tembele, mchicha, sukuma wiki, spinachi, bamia, karoti, matango, figili na nyingine nyingi, katika kundi hili mgonjwa anatakiwa kutumia kwa wingi kulingana na uwezo wake.
Kundi la nne ni Mtunda; Mgonjwa wa kisukari anatakiwa kula matunda  kwa kiasi
kidogo ila kila siku, maembe,mananasi, ubuyu,machungwa, mapera, zambarau na mengine mengi.
Nakuongeza kuwa mgonjwa wa kisukari anatakiwa kupendelea kula matunda zaidi kulikuyatengenezea juisi jambo linasabaisha kupunguza virutubisho vinavypatikana kwenye matunda, pia atakiwi kula muwa.
Kundi la tano ni mafuta na sukari;mgonjwa wa kisukari anatakiwa kutumia mafuta ya kupikia yatokane na mimea na siyo wanyama (mbegu zitoazo mafuta kama ufuta, korosho, kweme, alizeti na karanga, kwa kiasi kidogo), pia asitumie sukari ya aina yoyote.
Hata hivyo anasema kuwa mgonjwa wa kisukari anatakiwa kupunguza ulaji wa chumvi, mafuta na sukari, pia wasipende kutumia vitu vya kiwandani.
Vilevile  anaeleza kuwa mgonjwa wa kisukari anatakiwa kuzingatia kupta milo 6,kwa sikuambayo 3kamili na mingine 3 midogo.
Mhana anasema mgonjwqa wa kisukari anapaswa asubuhi apate chai ya maziwa, uji wa lishe au mahindi ambayo hayajakobolewa, lakini visiwe na sukari pamoja na vipande viwili vya mkate.
Saa nne asubuhi kula kidogo, tunda kama embe au chungwa moja, kikombe cha uji na kadhalika. Saa 7 mchana kula chakula kamili kama ugali, wali, viazi hku ukiweka kiasi kikubwa cha mbogamboga, bila kusahau tunda kama papai, parachichi robo kipande pamoja na ndizi mbivu moja.
Saa kumi jioni kula kidogo kama  chai au maziwa kikombe kimoja na kitafunwa chochote lakini kisiwe na sukari,saa kumi na mbili jioni unakula kachumbali, mbogamboga na matunda kama chungwa 1.
Pia muda wa saa 2 au 3  unakula mlo kamili kama wali, ugali, ndizi kwa kuzingatia usawa wa ngumi huku ukiweka mboghamboga kwa wingi na amatunda.
Pamoja na kuzingatia mlo hulaji huo mgonjwa wakisukari anapaswa kunywa maji kwa kiwango kikubwa ili kusaidia mzunguko wa damu na kupunguza sukari mwilini.
Mhana anasema kuwa mazoezi kwa mgonjwa wa kisukari ni muhimu, hivyo anatakiwa  kuruka kamba , kucheza mziki, mpira, jogging kwa nusu saa angalau mara nne hadi tano kwa wiki na unatakiwa ufanye ukiwa na ndugu au rafiki, kisha tembea na kitambulisho chako ili kukusaidia wakati umepata matatizo.
Pia wakati wa kufanya mazoezi unatakiwa utembee na glucose au sukari kwa ajili ya dharura,kwani unapofanya mazoezi bila kula inapelekea kushuka kwa sukari.
Inatakiwa mgonjwa kufanya yote na kuzingatia  utumiaji wa dawa jambo litakalosaidia kuishi maisha marefu.

Mhana anasema kuwa jambo linalopeleka mgonjwa anakatwa miguu ni kutokuwa na elimu kuhusu ugonjwa  na kutofata mashariti,hivyo serikali na wadau mbalimbali wenye ufahamu kuhusu kisukari watumie muda mwingi kuwaelimisha.
Pia aliwataka wagonjwa kufata mashariti mpangilio wa chakula, mazoezi, matumizi sahihi ya dawa na sindano za Insulini, na jamii kuacha kuwa wavivu wa kufanya mazoezi ata kama haja athirika na kisukari pamoja na ulaji wa  vyakula vya kusindikwa viwandani. 
Itaendelea, Imeandaliwa na Judith Ferdinand; 0757804962 Kwa msaada wa mtandao na mashirika ya habari.

No comments:

Powered by Blogger.