LIVE STREAM ADS

Header Ads

WAKAZI WA MWANZA WATAKIWA KUZINGATIA UTUNZANI WA MAZINGIRA.

Na:Vesterjtz,Mwanza 
Wakazi wa Mkoa wa Mwanza wametakiwa kutunza mazingira ili kujikinga na maradhi ya milipuko ukiwemo ugonjwa wa kipindupindu hususani katika msimu huu wakipindi cha mvua na msimu wa maembe.

Akizungumza jana, Mratibu wa mradi wa Mwanza Tampere na Mazingira Amin Abdarah alisema jamii imekuwa ikishindwa kutunza mazingira ipasavyo na kusababisha magohnjwa ya milipuko  hususani gonjwa la kuhara.

“Jukumu la kutunza mazingira ni la kila mtu na sio serikali pekee,magonjwa ya mambukizi kama kipindupindu ni jukumu la kila mwananchi kuhakikisha Tanzania inaondokana na magonjwa yanayoepukika,”alisema Amini.
 
Hivyo jamii inapaswa  kuzingatiumuhimu wa usafi   na kuwepo kwa maji safi ya kunywa kusafisha vyombo kwa maji safi na salama kutumia sabuni kwa kunawa mikono,uhifadhi wa chakula na  vyoo bora na kusafisha maeneo yanayowazunguka.

Aidha maradhi ya kipindupindu yamewahi kuripotiwa mara nyingi kuzuka sehemu mbalimbali duniani kulingana na shirika la afya ulimwenguni WHO watafiti wanakadilia kuwa kati ya watu milion1.4 hadi milioni 4.3 huripotiwa kuugua kipindupindu  huku elfu 142 hupoteza maisha kila mwaka kwa ugonjwa huo ambao huwaathiri watoto na watu wazima.
Mwisho.

No comments:

Powered by Blogger.