MWILI WA MAWAZO SASA KUAGWA JIJINI MWANZA.
Zuio la Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza lililotolewa na Kamanda wa
jeshi hilo Charles Mkumbo mwishoni mwa wiki iliyopita kwa madai ya kuwepo na
hofu ya kiusalama pamoja na uwepo wa mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu, hatua
iliyosababisha Mchungaji Charles Lugiko ambae ni baba mlezi wa Marehemu Mawazo
kwa kuungwa mkono na Chadema kufungua kesi ya msingi katika Mahakama Kuu Kanda
ya Mwanza ili kuiomba mahakama hiyo kuondoa zuio hilo.
Baada ya
Mawakili wa pande zote mbili zilizokuwa zinahusika katika kesi hiyo ambayo
ilifunguliwa juzi, Jaji wa Mahakama hiyo Lameck Mlacha akaamua kutengua zuio la
polisi alilosema kuwa halikuzingatia haki.
Kufuatia
maamuzi hayo, Mahakama ikashauri kuwa ni vyema ndugu wa marehemu Mawazo wakashirikiana
na Chadema pamoja na jeshi la polisi ili kuratibu shughuli za ibada ya kuuaga
mwili wa Marehemu Mawazo kwa ajili ya kuhifadhiwa, ikizingatiwa kwamba ni
takribani siku 12 mwili huo umehifadhiwa katika hospitali ya Rufaa Bugando.
Mwenyekiti
wa Chadema Taifa Freeman Mbowe amesema kuwa maamuzi hayo yataheshimiwa na
kwamba taratibu za kuuaga mwili wa Marehemu Mawazo zinafanyika ili ikiwezekana
mwili huo uweze kuagwa kesho ijumaa Jijini Mwanza.
Inje ya
viunga vya Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, ilikuwa ni nderemo na vifijo baada ya
Mahakama kutoa hukumu ya kesi hiyo ambayo imevuta hisia za wakazi wengi wa
Jijini hapa huku hali ya ulinzi na usalama wa polisi wa kutuliza ghasia
waliokuwa na silaha za moto pamoja na mabomu ya machozi ikiwa imeimarishwa kila
kona Jijini Mwanza.
No comments: