LIVE STREAM ADS

Header Ads

HILI NALO NI JIPU LASUBIRIWA KUTUMBULIWA. NI TANESCO KUPUUZIA WITO WA WANANCHI, KUHUSIANA NA NGUZO HATARISHI.

Wananchi wa Eneo la Tegeta Nyuki Jijini Dar es Salaam wamelilalamikia Shirika la TANESCO kushindwa kutatua Kero ya Nguzo ambayo inahatarisha Maisha ya wakazi Hao katika eneo hilo kwa zaidi ya Miaka 8 hivi sasa, nguzo hiyo imesogelea Kibanda cha Biashara na kusababisha hali ya Sinto fahamu kufuatia usalama wao.
Uzembe wa Nani?

Wakizungumza na Mtandao huu wakazi wa Eneo hilo wamedai yakuwa Taarifa walisha peleka katika sehemu husika lakini Hadi leo hii ni mwaka wa Nane Bila ya Mafanikio.
Uzembe wa Nani?
Mwaka 2008 wakazi hao waliiandikia Tanesco Barua ya kufanya Marekebisho ya Kuomba Kuondoa Mstimu huo lakini hadi leo Mamlaka hiyo haijafanya hivyo, Ila Mwaka 2015 mwishoni Tanesco ilifika eneo la tukio na kuangalia tu na kuondoka bila ya kufanya Marekebisho yoyote.
Uzembe wa Nani?
Je kwa hali hii Tunangojea Maafa au Hasara Itokee Ndio tukimbilie? Tunaiomba Mamlaka Husika Iweze Kuchukua Hatua za Haraka kurekebisha hili kabla ya Maafa hayajaweza Kutokea.

No comments:

Powered by Blogger.