LIVE STREAM ADS

Header Ads

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI: TAMKO LA WARATIBU WA CHASO MIKOA.

                              CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA).
         CHADEMA STUDENTS’ ORGANIZATION (CHASO).

TAMKO LA WARATIBU WA CHASO MIKOA
Ndugu zangu waandishi, habarini, tumewaiteni hapa ili muweze kutusaidia kuupeleka ujumbe huu kwa watanzania na wahusika.
Kwanza tunaunga mkono tamko la kamati kuu ya chama lililotolewa jana na mwenyekiti wa chama kwa vyombo vya habari.

1.    UCHAGUZI WA MEYA WA JIJI LA DAR ES SALAAM
Kwanza tunasikitika takribani siku zaidi ya 100 zimepita tangu kufanyika uchaguzi mkuu 2015, wa urais, wabunge na madiwani lakini cha kushangaza jiji la Dar es Salaam mpaka leo halina Meya ambapo kisheria ilipaswa awe amepatikana ili akawahudumie wananchi lakini tunashuhudia matumizi makubwa ya vyombo vya dola dhidi ya madiwani na wabunge wa UKAWA.

Tumeshuhudia RAS wa mkoa wa Dar es Salaam akitumia amri bandia ya mahakama kwa kukwamisha uchaguzi usifanyike, lakini hajachukuliwa hatua za kisheria mpaka sasa. Tunavitaka vyombo vinavyohusika vimchukulie hatua mara moja, vinginevyo tutaendekeza upotoshwaji na uvunjwaji wa sheria katika nchihii.

Pia tunawataka wenzetu wa CHAMA CHA MAPINDUZI wakubali kushindwa na waheshimu maamuzi ya wananchi wa Dar es Salaam waliowachagua kwa wingi madiwani na wabunge wa UKAWA ili waliongoze jiji la Dar es Salaam kwa miaka mitano ya kikatiba.

Tunahimiza uchaguzi huu ufanyike haraka ili wananchi wa Dar es Salaam wapate haki ya kutatuliwa kero mbalimbali, kupitia viongozi waliowachagua. Pia tunalitaka jeshi la polisi liache kuwanyanyasa na kuwadhalilisha madiwani na wabunge wetu, kama ambavyo wamefanya Kilombero, Dar es Salaam, Kyerwa na Zanzibar.

2.    HALI YA ELIMU NCHINI
Ndugu zangu waandishi wa habari tumeshuhudia hivi karibuni, wizara ya elimu kupitia tume ya vyuovikuu nchini (TCU) ikivifutia usajili baadhi ya vyuovikuu nchini, kama vile matawi ya St. Joseph Songea na Arusha, na baadhi ya vitivo katika Chuo Kikuu cha Kampala Dar es Salaam.

Hivi ni viashiria vya anguko la elimu nchini, tunahoji ni kwanini TCU awali ilikubali kuvisajili vyuo hivi na baadae kuvifuta? Je vyuo hivi vinafutiwa usajili kwa sababu havijakidhi vigezovya kuwa vyuo vikuu? Kama ni ndiyo,vyuo hivi vimezalisha wataalamu wasiokidhi vigezo katika kada mbalimbali, hivyo tunavitaka vyombo vinavyohusika kuwachukulia hatua za kisheria tume ya vyuo vikuu Tanzania (TCU) mara moja kwa kuhusika moja kwa moja katika maporoko ya elimu Tanzania.

Jambo hili limesababisha usumbufu kwa wanafunzi katika vyuo hivi, tunaitaka serikali ichukue hatua za haraka kuwasaidia wanafunzi hawa kupata vyuovingine navile vile iwalipe fidia kwa usumbufu uliojitokeza.

Vile vile tunaiomba serikali kupitia wizara ya elimu kuangalia upya mfumo wa utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu, ni wazi kwamba fedha hizi haziwanufaishi wanafunzi wanaotoka katika mazingira magumu kuweza kugharamia elimuyao, vile vile serikali ichukue hatua za haraka kuwasaidia wanafunzi wasio na mikopo vyuoni ili waweze kupata haki yao ya kupata elimu.

Suala la elimu bure bado ni changamoto, kwani pesa zilizotolewa kwa awamu ya kwanza hazikuweza kukidhi utoajiwa elimu katika shule mbalimbali hapa nchini, kwa mfano shule ya msingi Chiseyu iliyopo Mpwapwa Dodoma yenye wanafunzi zaidi ya 780 ilipewa kiasi cha Tshs 29,000/=, kwa mazingira hayo ni wazi kwamba sera hii itadumaza hali ya elimu, lengo la watanzania siyo kupata elimu bure tu, bali iwe bure na bora, ili elimu iwe bora serikali inapaswa kuchukua hatua malimbali kwa mfano kuimarisha miundombinu ya elimu (mishahara inayokidhi mahitaji ya mwalimu, vifaa vya kufundishia na kujifunzia vilivyo bora).

Serikali itoe onyo kwa Chama cha Mapinduzi kuingilia Maamuzi ya vyuoVikuu, kwa mfano hivi karibuni tumeshuhudia Chama cha Mapinduzi kikishinikiza Chuo kumfukuza Mwanafunzi wa Chuo kikuu cha Dodoma, Victor A. Byemelwa  kupitia kwa mshauri wa wanafunzi (DEAN OF STUDENTS) kwa barua yenye kumbukumu no Re.UDOM/DOS/36 ya tarehe 5 february 2016.

Imetolewa leo tarehe 06/03/2016 Makao Makuu CHADEMA
Na: JAFARY NDEGE, MWEKITI

K.N.Y: WARATIBU WA CHASO MIKOA YOTE TANZANIA

No comments:

Powered by Blogger.