LIVE STREAM ADS

Header Ads

VIONGOZI MWANZA WATAKIWA KUWAJIBIKA ILI KUENDANA NA KASI YA RAIS MAGUFULI.

Judith Ferdinand, Mwanza
Viongozi mbalimbali Mkoani Mwanza wameombwa kumuunga mkono Rais John Magufuli, katika  kuwatumikia wananchi   kwa  uadilifu, mshikamano, kujituma, kujitoa  pamoja na kuwajibika ipasavyo kiutendaji. 

Wito huo ulitolewa jana na Diwani wa  viti maalum  Wilaya ya Ilemela (CCM), Kulthum Abdallah, wakati akizungumza na majira katika ofisi ya kata ya Nyamanoro wilayani hapo.

Abdallah alisema, viongozi wanatakiwa kuwajibika, kushirikiana  na kujitoa bila kujali itikadi ya vyama, dini wala kabila, kwa kuhakikisha ahadi walizotoa wakati wa kampeni, wanazitekeleza ili kwenda na kasi ya rais sambamba na kumuunga mkono   katika suala la kutumikia wananchi.

Pia alisema, viongozi wanatakiwa kukaa na jamii pamoja na vijana kwa ajili ya kuweka mikakati ya jinsi gani wataweza kujiajiri sambamba na kuwaajiri wengine kwa kutumia mbinu mbalimbali,  ili kujikomboa kiuchumi na kuacha kuwa tegemezi  kwa familia na taifa. 

Alisema,  ni wajibu wa viongozi na wazazi  kushirikiana katika suala zima la  kuwaelimisha  vijana wanaotumia madawa ya kulevya, ili waweze kuacha na kubadilika, kwani itasaidia kuwakomboa kutokana na kupoteza muelekeo wa maisha.

Hata hivyo alisema, watashirikisha wadau mbalimbali sambamba na kutafuta wadhamini,  ili kuleta maendeleo  na kutatua changamoto zinazowakabili wakazi katika kata zilizopo wilayani humo, kwani viongozi na serikali pekee haiwezi.

Vilevile alisema, wameanzisha mabaraza ya watoto pamoja na mtandao wa watoto wanahabari katika kata ya Nyamanoro  kupitia  Diwani wa kata ya Nyasaka Shabani Maganga, ambao umelenga kugusa  wilaya nzima, kwa ajili ya kuwafundisha na kuwaelimisha masuala mbalimbali sambamba na kuoimba halmashauri kutenga fedha kwa ajili ya mabaraza hayo.

No comments:

Powered by Blogger.