LIVE STREAM ADS

Header Ads

CHADEMA MKOANI MARA WATOA KAULI KUHUSIANA NA BUNGE KUTOONYESHWA LIVE.


Katibu waChadema Mkoa wa Mara, Chacha Heche (katikati) akiwa na madiwani wa halmashauri ya Tarime Vijijini nje ya ofisi ya mbunge wa jimbo la Tarime Vijijini (Chadema).
Na:Binagi Blog

Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, kimesema hakikubaliani na uamuzi wa matangazo ya shughuli za bunge kutorushwa moja kwa moja (live), kwa kuwa hatua hiyo inawanyima wananchi kupata taarifa na habari sahihi za bunge.

Katibu wa Chama hicho Mkoani Mara Chacha Heche, ameyasema hayo hii leo katika ofisi ya mbunge wa jimbo la Tarime Vijijini, wakati akitoa taarifa kwa wanahabari kuhusiana na mwenendo wa uendeshaji wa shughuli za bunge ambao amesema kuwa umekosa mwelekeo.

“Katika awamu hii ya tano, ya Serikali inayojinasibu kuwa ni ya utumbuaji wa majipu tumeona ukiukwaji mkubwa wa katiba ya nchi na sharia mbalimbali ikiwemo kitendo cha serikali hii kuamua kwa makusudi kuwaficha wananchi kupata habari kutoka katika mhimili wao pekee ambao jukumu lake ni kuwawakilisha wananchi”. Amesema Heche.

Aidha amehoji ni kwa nini serikali inayojinasibu kuwa ni ya utumbuaji majipi, inataka majipu hayo yatumbuliwe gizaji, huku nguvu kubwa ya dola ikitumika kuwazima wawakilishi wanaotetea wananchi wao waone ili waone namna wanavyotenda kazi zao wawapo bungeni.

Heche ameenda mbali na kuhoji zaidi ni kwa nini hata vyombo binafsi vya habari vimezuiliwa kurusha live matangazo ya shughuli za bunge ikizingatiwa kwamba taarifa iliyotolewa awali na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh.Nape Nhauye ya kutorusha matangazo hayo live kupitia shirika la taifa la utangazaji TBC ni uhaba mdogo wa gharama za uendeshaji.


“Rais wa awamu ya utumbuaji majipu alisema mwenyewe atawatumbua watendaji wa serikali mchana kweupe kwa kuwa aliwateua yeye tena na kuwatangaza hadharani, sasa iweje sisi wananchi ambao tuliwachagua wabunge wetu kwa kura mchana tuonyweshwe wanachojadili usiku, tena kipindi kilichorekodiwa wakati sisi tuliwachagua live baada ya kuwasikiliza live”. Amehoji Heche. 

No comments:

Powered by Blogger.