LIVE STREAM ADS

Header Ads

SERIKALI YAAHIDI KUWASAIDIA WAJASIRIAMALI WA MAZAO YA NGOZI NCHINI.

Judith Ferdinand, Mwanza
Serikali imejipanga kusaidia  wajasiriamali pamoja na vyuo vinavyotoa elimu ya ujasiriamali   wa kutumia malighafi   za ngozi za wanyama, ili kuendeleza sekta ya ngozi ili kutoa ajira kwa vijana.

Kauli  hiyo imetolewa jana  na Katibu Mkuu Biashara na Uwekezaji, Prof. Adolf Mkenda, wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya ujasiriamali wa kutumia ngozi katika chuo cha Dar es Salaam Institute of Technology (DIT) tawi la Mwanza.

Prof. Mkenda alisema, ili kuzalisha bidhaa bora za ngozi, inatakiwa vijana kupatiwa mafunzo yatakayosaidia kuendana na soko   la kimataifa.

Mmoja wa wajasiriamali waliohudhuria mafunzo hayo Thobias  Machele, amesema katika sekta ya uzalishaji bidhaa kwa kutumia ngozi wanakabiliwa na ukosefu wa mashine ambao ungesaidia  kuokoa muda na kutoa vitu vilivyo bora.

No comments:

Powered by Blogger.