MBUNGE VITI MAALUMU MKOANI IRINGA KUWAPIGA MSASA WANAWAKE.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoani Iringa, Rose Twelve, akifurahi jambo na akinamama wenye ulemavu Mkoani humo.
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Rose Twelve akizungumza na wanawake wa chama cha mapinduzi ccm mkoani iringa.
Na Fredy Mgunda, Iringa
Wananchi Mkoani Iringa wanatarajia kunufaika na Muungano
wa Wabunge Watatu Vijana wa Viti Maalumu Mkoani humo, kwa lengo kubadilishana uzoefu wa
kuwaletea Maendeleo Wanawake Mkoani Iringa.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa Iringa, Rose Twelve, amesema wameamua
kuungana ili kubadilisha mfumo wa utawala na kuondoa ufanyaji wa kazi kwa
mazoea sambamba na kuwasaidia wananchi wanaowatumikia.
“Unajua kuwa changamoto na matatizo ya wanawake kwa
asilimia kubwa zinafanana hivyo najifunza kwa wenzangu wanatatuaje changamoto
hizo ili na mimi niweze kutatua matatizo ya wanawake wa mkoani iringa na
waendelee kufanya maendeleo huku wakiwa hawana changamoto nyingi”. Alisema Rose
“Nitatoa milioni hamsini kila mwaka kwa umoja wa Wanawake
wa CCM UWT Mkoani hivyo lazima nitafute njia mbadala ya kuwapa elimu ya
kuzitumia hizo pesa ili ziwanufaishe kwa kuwaletea maendeleo”.alisema Rose
Rose alisema kuwa atatafuta wataalamu wa mafunzo
mbalimbali ili wanawake wa Mkoa wa Iringa wapate elimu ya ujasiriamali na
kuokoa pesa ambazo zimekuwa zikipotea.
"Nitatafuta wadau mbalimbali wachangie mfuko wangu wa
mbunge kwa lengo la kuwasaidia wanawake ambao hawana mitaji ya kujiendesha
maisha yao". Alisema Rose huku akiwataka wakazi wa Iringa kufanya kazi kwa
bidii ili kuleta maendeleo binafsi na taifa kwa ujumla.
No comments: