SOMA UCHAMBUZI MAALUMU KUHUSU SERA YA MAENDELEO YA VIJANA NCHINI TANZANIA.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Edwin Soko ambae ni Mchambuzi na Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari wa Matumizi ya Dawa za Kulevya na Uharifu. Pia ni Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoani Mwanza. (Picha Kutoka Maktaba-BMG)
1:Nini Maana
ya Sera?
Ni
mpango, hunaoweza kuandaliwa na serikali, chama cha siasa au biashara ikiwa inalenga kutoa ushawishi utakaopelekea kufanywa kwa
maamuzi , vitendo na hatimaye
kupata mafanikio.
Sera
ta Taifa ta
Maendeleo ya Vijana
inatoa mwongozo si tu
kwa vijana, wazazi na waelimishaji bali kwa
jamii nzima na hasa
kwa wapangaji wa mipango
ya maendeleo katika
sekta mbalimbali za maendeleo.
2:Maana ya kijana
Inaweza kutofautiana
kutokana na mila, desturi na
tofauti za maadili katika jamii mbalimbali
na mahali walipo. Kijana ni
mvulana au mwanamke ambaye
yupo katika rika la utoto
kuelekea rika la utu uzima. Kuligana na
tofauti mbalimbali sera
hii imetumia fafsiri
ya kijana kutokana na tamko la Umoja wa Mataifa ambapo kijana ni mtu
mwenye umri kati ya
miaka 14- 24.
3:Historia hadi
kutungwa kwa Sera
Tangu
Tanzania ipate uhuru
wake mnamo mwaka 1961
hapakuwa na Sera rasmi iliyoandaliwa
kwa ajili ya
malezi na maendeleo ya
Vijana . Masuala ya malezi na maendeleo ya
vijana kwa kipindi chote hicho
yalikuwa yakitekelezwa kupitia
Sera nyingine katika mipango ya
maendeleo, kampeni, maazimio na
miongozo ya chama tawala na
Serikali.
Sera hii iliandaliwa kwa ajili ya kusimamia maslahi ya kijana, ambayo serikali iliandaa mwaka 1996 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2007, Sera ya taifa ya maendeleo ya vijana ya 2007 inalenga masuala ya maendeleo ya vijana ambayo ni pamoja na: uwezeshaji wa kiuchumi, mazingira, VVU na Ukimwi, jinsia, sanaa na utamaduni, michezo afya ya uzazi kwa vijana na masuala ya maisha ya familia.
4:Msingi
wa Sera
Msingi wa sera unatokana na uzingatiaji wa haki za binadamu
kama zilivyotajwa katika katiba
ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977
na kufanyiwa marekebisho mwaka 1984 na 1995. Haki
hizi ni pamoja na haki
ya kuishi, kulindwa,
kuendelezwa na kujiendeleza,
kushirikishwa katika shughuli za maendeleo yake
na jamii. Haki nyingine
kulingana na katiba hiyo ni pamoja na
haki ya kutobadiliwa ,
kuheshimiwa, kumiliki mali na rasilimali, kufanya kazi
na kupokea matunda
ya kazi hiyo pamoja na mbele ya sheria
za Nchi.
4:Lengo la
Sera
- Kuhakikisha Taifa linakuwa na
vijana wenye uwezo, wenye ari ya kutosha , wawajibikaji na wanaoshiriki
kikamilifu katika Nyanja zote za kijamii, kisiasa na kiuchumi kwa
maendeleo ya jamii.
- Kuweka mazingira yanayowezesha kujenga uwezo wa vijana na kukuza nafasi za ajira na kupata huduma ya hifadhi ya jamii
5:Uchambuzi
Sera ina sehemu
kuu Tano (5)
5:1 Sehemu ya kwanza:
Hii inaeleza
utangulizi kwa mujibu wa miongozo
ya kisera
5:2 Sehemu ya pili:
·
Umuhimu wa sera
·
Dhamira
·
Dhima
·
Malengo
5:3 Sehemu ya Tatu
Sehemu hii imebeba mambo (29)
yakiwemo:
- Mambo kisera na maelezo yake
- Tafsiri sahihi ya
kijana
- Mzingira ya vija
kuishi kwenye dimbwi la matatizo
- Maandalizi ya kijana
ili aishi kwa kufuata
misingi ya jamii
- Rasilimali zinazoweza
kumwinua kijana na kumwendeleza
- Huduma za kifedha zninazoweza kuondoa umaskini kwa kijana
- Ushiriki wa vijana
kwenye kilimo na
ufugaji
- Nafasi za vijana
kwenye serikali za
mitaa na uongozi wa Mkoa
- Haki za kijana
- Misingi ya usawa wa
kijinsia kwenye maendeleo
- Mifumo ya
kisheria ya kumwendeleza kijana
- Vijana na sekta
ambazo si rasmi
- Chombo cha kisheria
cha kuwaunganisha vijana
- Ushiriki wa kijana
kwenye kumwelndeleza kijana
- Kijana na fursa
za ajira
- Vijana na madhira
ya Ukimwi
- Matumizi ya
TEHAMA Kwa vijana
- Kijana na ulemavu
5:4 Sehemu
ya Nne
-Majukumu ya wadau
- Wazazi na walezi
- Mashirika ya dini, taasisi
zisizo za kiserikali, sekta binafasi
na asasi za kijamii
- Serikali za Mitaa na
uongozi wa Mkoa
- Serikali kuu
- Wadau wa maenedeleo
5:5 Sehemu
ya Tano:
-Mpangilio wa utekelezaji
-Hupatikanaji wa huduma za kijamii
-Usimamizi wa
program, ufutiliaji na tathimin
6:0 Mtazamo
Kimsingi Suala
la Taifa kuwa
na sera ya
Vijana limechelewa kwa
kiasi kikubwa kwani tumepata sera
hiyo mwaka 2007
wakati wenzetu Kenya ilikuwa
na sera hiyo mwaka …………….
Uganda mwaka ……………..
Mwanasisasa Zitto
Kabwe hakukosea kusema
kuwa Taifa hili ni
Taifa la Vijana na watoto, kwani kwa mujibu
wa sensa ya
watu na makazi
Vijana wamebeba asilimia
33/% ya watu
wote.
Vijana na
Uchumi wa Nchi
Nchini Tanzania
vijana wengi wamekuwa
wakijihusisha katika sekta
za kilimo, uvuvi, madini, ufugaji
na uwekezaji kwenye viwanda
vidogovidogo kama utengenezaji wa matunda, vitua
asilia na vinginevyo.
UCHAMBUZI
Kwa
kiasi kikubwa sera
imeakisi matatizo ya
vijana wa kitanzania na
pia kutoa mwelekeo
mzuri sana wa kuyashughulia matatizo
hayo.
Mfano:
Suala la
ajira kwa vijana
Kama tujuavyo
kuna vijana wengi
wanaomaliza elimu ya msingi, sekondari na
vyuo vya juu
wakikosa ajira na kuangukia kwenye sekta
zisizo rasmi, ambazo huko
hakuna job security, kukosekana kwa mitaji
Kauli ya
sera
- Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi itaandaa mazingira mazuri ya kutengeneza ajira kwa vijana.
- Kuwa na sera ya Taifa ya ajira
- Kuwa na sera ya undelezaji maeneno ya vijijini na kilimo (Rural Development Strategy and Agricultural Development Policy.
- Serikali kushirikiana na taasisi binafsi na wadau wengine kutoa elimu ya ujasiriamali kwa vijana ili waweze kujiajiri.
Ushirikishwaji
wa vijana na
Utawala Bora
Vijana wanamchango
wa 65% ya nguvu kazi
ya wazalishaji wa uchumi wa
Taifa (Labour Force) lakini
35% ya vijana
hao hawawakilishwi vyema kwenye
forums mbalimbali za ngazi ya
maamuzi, na matokeo yake maamuzi
mengi yanayofikiwa hayagusi matatizo
ya vijana.
Kauli ya sera
Mifumo ya
halamashauri za serikali za
mitaa na
serikali kuu iwe na
mifumo inayotambua uwepo wa jina
na pia uwakilishi
kwenye ngazi nyingine
za kitaifa na kimataifa
Kuwa na
chombo cha kuwaunganisha vijana
Kwa
muda mrefu kulikuwa
hakuna chombo chenye
nguvu kinachoweza kuwaleta vijana
pamoja na kutambua matatizo yao.
Kauli ya
sera
Kuundwa kwa
chombo kitakachoweza kuwasemea
vijana “ Uuundwaji wa Baraza
la Vijana Taifa”
Huduma za kifedha
na mkakati wa kupunguza umaskini
Kuna mikakati mingi iliyopitishwa
kwenye kuwainua vijana kwa kuwapa misaada ya kifedha
ili waweze kujiinua kiuchumi, lakini mikakati hiyo
imekuwa si endelevu, wala mpangilio
mzuri
Kauli
ya sera
- Kuwa na mkakati endelevu
wa kuwasaidia vijana kifedha ili waweze kujiinua kiuchumi
- Kusisitiza umuhimu wa kuwa na mfuko wa wa fedha wa kuwasaidia vijana.
Nafasi ya
vijana kwenye muundo wa
Serikali za mitaa
Muundo
wa Serikali za mitaa
hakuweza kuwa na uwakilishi
mzuri wa kutambuamatatizo ya vijana, kwa kuwa hakukuwa
na Afisa anayeshughulikia uendelezi
wa kada ya vijana, hii
ilifanya kuwa na mfumo
dhaifu toka serikali
kuu hadi serikali
za mitaa.
Kauli
ya Sera:
- Kuwe na up -
down approach wa kutoa uwakilishi toka
ngazi za kata hadi
Taifa, hilo liwe jukumu
la wizara husika
ya serikali za mitaa na
serikali kuu
- Serikali kuu na serikali za mitaa iweke utaratibu wa kuajiri Afisa atakayehusika na undelezaji wa kada ya vijana
Vijana kuishi
kwenye mazingira magumu
Kuna vijana
wapatao million 2
yatima wanaoishi kwenye mazingira
magumu sana ya kimaisha
Kauli ya sera
Sera imeelekeza kuwa, kuna mkakati
wa kuwawezesha kupata fursa
kwenye elimu, mafunzo na
usalama wao kwa wote waliokubwa na
matatizo hayo.
Maandalizi kwa kijana
ili awe raia
mwema kwenye jamii
Vijana wametakiwa
kuwa na maandalizi
mazuri ili waweze kutimiza
wajibu wao kwenye jamii wa kuwa
raia wema.
Kauli
ya sera
Kuwa na
mkakati maalumu wa kuandaa
miongozo ya malezi
kwa vijana
Matumizi ya
rasimimali za Nchi zinazoweza
kuwainua vijana
Tunaelewa wote
kuwa Nchi yetu ina rasilimali nyingi, ambazo zikitumika
vizuri zinaweza kuwasaidia sana vijana
kuinua maisha yao.
Rasilimali hizo ni
kama ardhi na nyinginezo
Kauli ya
sera . Kwa mujibu wa integrated labour
survey 2001, asilimia 65
ya wazalishaji wa
uchumi wa Nchi ni Vijana.
Kauli ya
sera
Kutakuwa na
kipaumbele cha rasimimali za
Nchi kwa kundi la vijana
Matumizi
ya TEHAMA
Vijana
wengi wamekuwa wakitumia
teknolojia kwa mtazamo
hasi badala ya
chanya, kama kutumia kwa kukuza weledi wa kitaaluma wao
wanatumia kwa kutazama vitu
vinavyoweza kumomonyoa maadili ya
Taifa
Kauli
ya sera
Kuwa na
makakati wa kufuatilia maudhui
ya matumizi ya
teknolojia
Mapungufu/Gap
Sera yetu
ina mapungufu machache kama
kutoweka kipaumbele kwa makundi
maalumu, hii inasababisha
baadhi ya makundi
Kutopewa kipaumbele, Sera ya
maendeleo ya vijana
ya Kenya yenyewe
imeweka vipaumbele kwa makundi
maalumu ya vijana kama walemavu, waathirika wa HIV, wanawake, vijana wasio na ajira na
wale waliokosa fursa za kusoma.
HITIMISHO
Sera ya
Maendeleo ya vijana ni
nzuri kwani imeanisha
matatizo ya vijana
na kutoa njia sahihi
ya kuyashughulikia, tatizo
kubwa linalojitokeza hapa
ni kama matatizo
ya sera nyingine
za Nchi hii suala zima la
utekelezaji wa sera
(Implementation) tu.
Endapo Serikali
ya awamu ya
tano itaamua sasa
kuisimamia sera hii
kwa kuitekeleza ni wazi kuwa
kijana kada ya
vijana itaboreka na kutoa mchango
mkubwa kwenye falasa
ya seriklai ya
John Pombe Magufuli ya
kwenda kwenye uchumi wa kati wa
Viwanda.
Naomba kuwakilisha
Edwin
Soko
PhD Candidate
Kumbuka Soko amewasilisha Uchambuzi huu hii leo katika Kongamano la Vijana Wajasiriamali na Wawekezaji mkoani Mwanza. TAZAMA HAPA.
Kumbuka Soko amewasilisha Uchambuzi huu hii leo katika Kongamano la Vijana Wajasiriamali na Wawekezaji mkoani Mwanza. TAZAMA HAPA.
No comments: