VIJANA ACHENI DHANA POTOFU.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
George Binagi-GB Pazzo ambae ni Mwanahabari, Blogger na Mkulima.
Ipo dhana potofu kwa vijana wenzangu kwamba Kilimo ni Kazi
ya kujitesa na haiwafai.
Niwaambie tu kwamba, kilimo kinalipa na kilimo ni sekta
muhimu katika kutatua changamoto ya ukosefu wa ajira kwa vijana nchini.
Kijana usikimbilie mjini kuuza sura ikiwa huna uhakika wa
ajira za mjini. Mali iko shambani hivyo ni vyema ukajikita katika kilimo, tena
kilimo cha kisasa.
Sahau kuhusu changamoto zinazotukabiri wakulima. Jitume
zaidi na baada ya muda utaweza kusonga mbele kimaendeleo kupitia kilimo.
Usihofu kuhusu "bring bring" unazopenda. Mambo
yamebadilika. Fanya kazi kwa ratiba. Baada ya shughuli zako za kilimo, tupia
hizo "bring bring" zako.
Pamoja na kwamba mimi ni Mwandishi wa Habari/Mtangazaji na
Blogger, pia mimi ni Mkulima na najivunia hilo kwani najua faida za kuwa
mkulima.
Ewe kijana uliekosa ajira na umekimbilia mjini, baada ya
kusoma post hii, anza kupanga ratiba za kurudi kijijini kwenu ili ukajikite
katika kilimo, huko utanufaika maradufu zaidi kimaendeleo.
No comments: