LIVE STREAM ADS

Header Ads

BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI NACTE LAKUNJUA MAKUCHA YAKE.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Na James Salvatory, Dar es salaam.
Baraza la Taifa la ELimu ya Ufundi nchini (NACTE)  limevifutia usajili  vyuo vitano huku vyuo 41  vinavyotoa elimu ya ufundi bila kusajiliwa vikipewa wiki mbili  ya kujisajili wakati vyuo 175 nchini vikishushwa hadhi.

Mwenyekiti wa (NACTE), Mhandisi Steven Mlote, amesema baraza limekuwa likivitembelea  vyuo na kubaini mapungufu ambapo  kuna vyuo  vimekeua namna ya utoaji wa masoma ya vyuo hivyo.

"Kuna vyuo mchana ni chuo usiku ni bar, na kuna vyuo vinatoa mafunzo tofauti na usajili wao na kuna vyuo ambavyo havijasajiliwa na vinatoa mafunzo huku kukiwa kuna vyuo ambavyo muda wake umeisha wa usajili na havijaenda kubadilisha au kuongeza hadhi yake huku kukiwa na vyuo ambavyo havina waalimu wanaotambulika yaan wenye vibali."Amesema Mlote.

Baraza limetoa muda wa mwezi mmoja kwa vyuo 112 kutekeleza marsharti ya usajili na vyuo 52 kutekeleza masharti ya ithibati kwa mujibu wa sheria za uendeshaji vyuo vya ufundi nchini na vyuo vitakavyoshindwa kutekeleza agizo hilo vitafungiwa mara moja.

Mlote amewataka wazazi  waache kuwapeleka watoto wao kwenye vyuo ambavyo havina usajili kutoka Nacte na kama wanataka kupata vyuo ambavyo vimetimiza masharti yote watembelee tovuti ya Nacte au wafike ofisini jijini Dar es salaam na Mikoani na wanafunzi waliokuwa wanasoma vyuo vilivyofungiwa kuwasiliana na baraza kwa ajili ya kuwatafutia vyuo vilivyokamilisha usajiri.

Vyuo vitano vilivyofungiwa na Nacte ni State College of Health and Allied Sciences, Zoom Polytechnic College, Tabitha College, Financial Training Center pamoja na TMBI College of Business and Finance  vyote vya Dar es salaam.

No comments:

Powered by Blogger.