KAULI YA KASSIMU MAJALIWA NI CHANGAMOTO KWA LUMBESA YA DAGAA MWANZA.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Na: Neema Joseph, Mwanza
Kauli aliyoitoa Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa mwanzoni mwa mwaka huu juu yakatazo la lumbesa imekutana na changamoto kubwa kwa upande wa biashara ya dagaa Jijini Mwanza, kwani sheria ya vipimo sura namba 340 ya mwaka 1982 imeshindwa kuainisha ujazo rasmi wa kutumika.
Meneja wa Wakala wa Vipimo Mkoa wa Mwanza Hemed Kipengele amekiri uwepo wa mapungufu kwenye sheria hiyo, kwani licha ya sheria kuanisha vipimokwa mazao na bidhaa mbalimbali, zao la dagaa halikuainishwa, hali inayoleta ugumu wa kuthibiti biashara hiyo.
Naye, wafanyabiashara Enock Mussa Pamoja na Kadogo Masanyiwa kwenye Soko la dagaa la Kirumba wamekiri madhaifu ya sheria hiyo ni kutoainisha kipimo cha dagaa na kusababisha malumbano makubwa baina ya wauzaji,wanunuaji na wasimamizi wa sheria.
Sheria ya vipimo imeshindwa kuainisha zao la dagaa hali inayopelekea uwepowa malumbano kwenye usimamizi wa agizo la Serikali, baadhi ya wafanyabiashara, Restuta Luoga, Leonard Sprian, Jonathan Malaba na William Clemence wametoa mapendekezo yao ya kutaka sheria hiyo ifanyiwe marekebisho ili zao la dagaa liingizwe kwenye sheria ili kuleta usimamizi mzuriwa agizo la Mheshimiwa Kassimu Mjaliwa.
Makala hii imefadhilwa na mfuko wa Wakfu wa tasnia ya Habari Tanzania (TMF). Maoni na ushauri wasiliana na Mwandishi wa makala hii kwa namba 0765892256.
Na: Neema Joseph, Mwanza
Kauli aliyoitoa Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa mwanzoni mwa mwaka huu juu yakatazo la lumbesa imekutana na changamoto kubwa kwa upande wa biashara ya dagaa Jijini Mwanza, kwani sheria ya vipimo sura namba 340 ya mwaka 1982 imeshindwa kuainisha ujazo rasmi wa kutumika.
Meneja wa Wakala wa Vipimo Mkoa wa Mwanza Hemed Kipengele amekiri uwepo wa mapungufu kwenye sheria hiyo, kwani licha ya sheria kuanisha vipimokwa mazao na bidhaa mbalimbali, zao la dagaa halikuainishwa, hali inayoleta ugumu wa kuthibiti biashara hiyo.
Naye, wafanyabiashara Enock Mussa Pamoja na Kadogo Masanyiwa kwenye Soko la dagaa la Kirumba wamekiri madhaifu ya sheria hiyo ni kutoainisha kipimo cha dagaa na kusababisha malumbano makubwa baina ya wauzaji,wanunuaji na wasimamizi wa sheria.
Sheria ya vipimo imeshindwa kuainisha zao la dagaa hali inayopelekea uwepowa malumbano kwenye usimamizi wa agizo la Serikali, baadhi ya wafanyabiashara, Restuta Luoga, Leonard Sprian, Jonathan Malaba na William Clemence wametoa mapendekezo yao ya kutaka sheria hiyo ifanyiwe marekebisho ili zao la dagaa liingizwe kwenye sheria ili kuleta usimamizi mzuriwa agizo la Mheshimiwa Kassimu Mjaliwa.
Makala hii imefadhilwa na mfuko wa Wakfu wa tasnia ya Habari Tanzania (TMF). Maoni na ushauri wasiliana na Mwandishi wa makala hii kwa namba 0765892256.
Soma Makala nyingine HAPA
No comments: