LIVE STREAM ADS

Header Ads

MADALALI WALALAMIKIWA KUKWAMISHA KAULI YA KASSIMU MAJALIWA JUU YA LUMBESA.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com


Mwandishi, Neema Joseph (kushoto) akifanya mahojiano.
Na Neema Joseph, Mwanza
Baadhi  ya  wauzaji  wa  dagaa  kwenye  Soko la  Kirumba  Jijini Mwanza  wamewalalamikia  madalali  Sokoni  hapo  kukwamisha  vita   dhidi  ya  lumbesa   kama  ilivyotolewa   kwenye  tamko  la  Serikali  kupitia  kwa  Waziri Mkuu  Kassim  Majaliwa kwenye  katazo  la  lumbesa.

Bwana  Raphael  Nkiru ,  Halphan  Said, Rehema  Muddy na  Dionis Mafuru, wote wafanyabiashara kwenye  Soko  la Kirumba waliwalalamikia   madalali  wa  Sokoni  hapo  kuwa, wanakwamisha   utekelezaji wa  agizo  la  Waziri Mkuu  Kassimu  Majaliwa   katazo la  lumbesa.

“Kimsingi  baadhi  ya  madalali  wamekuwa    wakitumwa  na  wafanyabiashara  wakubwa  toka  Nchi za Kongo  na  Burundi  kuwanunulia    dagaa  visiwani  na  huko  wanatumia  vipimo visivyo  rasmi  kwenye  kununua  dagaa  na  kuwaibia  wakulima  licha  ya  katazo  la Serikali” walihitimisha   wafanyabiashara hao.

Bwana   Ben  John  dalali  sokoni  hapo  alisema kuwa, wapo  baadhi  yao ambao  wamekuwa   sio  waaminifu  hasa  wanapoenda  kununua  dagaa  visiwani, ila  yeye  anazingatia  maagizo  ya  serikali  hawezi  nunua  dagaa  kwa  mfumo wa lumbesa pia  kama wanakuja wateja wanaotaka  kununua dagaa kwa mfumo wa lumbesa huwa anawafukuza.

Naye  dalali    ambaye  hakutaka  jina lake  litajwe  alisema  kuwa, suala  la wao  kununua  dagaa  kwa  mfumo  wa lumbesa   halina  ushahidi  wa kutosha  linahitaji  muda  mrefu  ili  kupata  majibu sahihi.

Uchunguzi  uliofanywa  na makala  hii  uligundua   uwepo wa Madalali   wengi  Sokoni  hapo  ambao  wamekuwa  wakijihusisha  kuendesha  biashara  ya  dagaa  Soko la Kirumba   kwa kuwa  kiungo  kati  ya  wafanyabiashara  wakubwa  na  wauzaji  wa  dagaa, hali  hiyo  imekuwa  kero  kwa  wauzaji wa dagaa  kwani  wanaona  kuwa, wanaibiwa  kupitia Madalali hao  ili  kuwanufaisha  wafanyabiashara.

Makala  hii imefadhiliwa  na  Mfuko wa  Wakfu  wa Tasnia ya Habari  Tanzania (TMF).

No comments:

Powered by Blogger.