MAONESHO YA NANENANE MKOANI ARUSHA YANOGA.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Baadhi ya vijana waliofika katika banda la wizara ya Kilimo na Mifugo wakipata maelezo juu ya ufagaji wa ng'ombe wa kisasa maalumu kwa ajili ya maziwa kutoka kwa Dkt.John Mpinga kutoka Luti Campus Tengeru. Ni katika Maonyesho ya Nanenane yanayofanyika katika Viwanja vya Njiro mkoani Arusha. Picha na Gadiola Emmanuel |
Na Dickson Mulashani
Vijana nchini wamehimizwa kushiriki kikamilifu katika
shughuli za kimaendeleo ikiwemo kilimo ikiwa ni sehemu ya kujikwamua na
kuliletea Taifa maendeleo sambamba na kumuunga mkono Rais kwa kauli mbiu yake ya HAPA KAZI TU!.
Hamasa hiyo inadhihirika wazi kupitia kauli mbiu ya maadhimisho
ya siku ya wakulima maarufu zaidi kama
nanenane mwaka 2016 inayosema KILIMO, MIFUGO NA UVUVI NI NGUZO YA MAENDELEO,
VIJANA SHIRIKI KIKAMILIFU, HAPA KAZI TU”
ambapo kitaifa yataadhimishwa mkoani Morogoro.
Ikiwa ni siku za mwanzo,mwitikio wa wananchi unaonekana kuwa mzuri. Picha hizi ni kutoka viwanja vya nane nane vilivyopo Njiro mkoani Arusha . |
Mkulima wa zao la viazi vitamu akionesha namna viazi vinavyoweza kutengeneza bidhaa zaidi ya moja ikiwemo "tambi" na "crips"
Mboga aina ya kabichi zikiwa katika ubora wa hali ya juu
Hakika kilimo kinapendeza
Afisa wa kampuni inayojishughulisha na utengenezaji wa nishati kwa ajili ya matumizi ya nyumbani akielekeza namna mkaa unaotengenezwa kutumia pumba unavyofanya kazi
Mmoja wa waliotembelea banda la TAHA akiangalia kwa makini zao la Hoho iliyonona vyema ambayo ni sehemu ya mradi wa TAHA
Sehemu ya mabanda ya maonesho yalivyotawala katika viwanja vya nanenane Njiro mkoani Arusha
Wizara ya Maliasili na Utalii nao tayari wamepiga kambi katika viwanja hivyo
No comments: