KITUO CHA SHERIA NA HAKI ZA BINADAMU CHATAKA ADHABU KALI ITOLEWE KWA WANAOSHINDWA KUTOA MALEZI BORA KWA WATOTO.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Wafanyakazi wa LHRC wakijumuika na watoto wanaolelewa katika Makao ya taifa ya watoto wenye shida Kurasini jijini Dar es Salaam jana ikiwa ni sehemu ya kusherehekea miaka 21 tangu kuanzishwa kwake.
Na Dotto Mwaibale
Na Dotto Mwaibale
Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Dk. Helen Kijo-Bisimba (katikati) akiwasaidia watoto kukata keki kusheherekea miaka 21 ya LHRC.
Ofisa Mfawidhi wa Makao ya Taifa ya Watoto wenye shida Kurasini, Beatrice Lawrance, akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika Dar es Salaam jana ikiwa ni sehemu ya maadhimisho hayo.
*******************************
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimeiomba serikali kupitia wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, pamoja na na Wizara ya Katiba na Sheria, kufanya marekebisho ya Sheria ya Mtoto na kutilia mkazo malezi bora ya watoto ikiwemo kuweka kipengele kitakachotoa adhabu kali kwa familia itakayo shindwa kutoa malezi bora kwa watoto au kutelekeza familia.
Akizungumza katika maadhimisho ya miaka 21 ya kituo cha sheria na haki za binadamu, yaliyofanyika katika Makao ya Taifa ya Watoto wenye shida kilichopo Kurasini, Temeke Jijini Dar es salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa kituo hicho Dk. Helen Kijo-Bisimba alisema kuboreshwa kwa sheria hizo kutasaidia kupunguza wimbi la watoto wasio na makao maalumu wanao zagaa kuomba omba mitaani, na ameitaka jamii kushiriki katika kutatua tatizo la watoto wa mitaani linalozidi kushika hatamu kila siku.
Ofisa Mfawidhi wa kituo hicho, Beatrice Laurence ame kishukuru kituo cha sheria na haki za Nina damu kwakuona umuhimu wa kutoka misaada katika kuwa saidia watoto wanao lelewa hapo nakuwataka watanzania wengine badala ya kuelekeza nguvu zao pekee kwa wathirika wa tetemeko huko Kagera kuwa kumbuka na watoto yatima kwani nao wanayo kahitaji ya kibinadamu.
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kilianzishwa Septemba 26, 1995 kwa lengo la kufanya utetezi kwa watu wenye uhitaji sambamba na kulinda haki za binadamu nchini.
No comments: