LIVE STREAM ADS

Header Ads

SHIRIKA LA "NI HEKIMA PEKEE" LATAKA WATOTO WASIOJUA KUSOMA NA KUANDIKA KUSAIDIWA.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Na Judith Ndibalema, Mwanza
Jamii imetakiwa kushirikiana na Serikali pamoja na wadau mbalimbali wa elimu ili kuwanusuru watoto walio mitaani ambao hawajui kusoma wala kuandika Jijini Mwanza.

Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la Ni Hekima Pekee, linalowahudumia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi Jijini Mwanza, Onesmo Kajuna, ametoa rai hiyo wakati akizungumzia hatari inayowakabiri watoto hao ikiwa watakosa fursa ya kupata elimu.

Amesema ushirikiano wa karibu miongoni mwa jamii, serikali pamoja na wadau wote wa elimu, utasaidia mpango wa MEKWA unaolenga kuwafundisha watoto wenye umri mkubwa nchini kujua kusoma na kuandika kufikia malengo yake.


Kajuna ameongeza kwamba watoto wakipata elimu, watajiepusha na utumiaji wa dawa za kulevya, ndoa pamoja na mimba za utotoni hivyo jamii inapaswa kuhakikisha hakuna mtoto anayekosa fursa ya kwenda shule ikizingatiwa kwamba elimu ya msingi na sekondari nchini inatolewa bure.

No comments:

Powered by Blogger.