LIVE STREAM ADS

Header Ads

VIKUNDI VYA UJASIRIAMALI KATIKA MANISPAA YA ILEMELA MKOANI MWANZA VYANUFAIKA NA FEDHA ZA MFUKO WAJIMBO.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Judith Ferdinand, Mwanza
Vikundi 20  vya ujasiriamali vya wanawake na vijana katika halmashauri ya Manispaa ya Ilemela mkoani mkoani Mwanza, vimenufaika na fedha za mfuko wa jimbo lengo likiwa ni kuvisaidia kujikwamua kiuchumi kupitia miradi yao.

Meya  wa  Manispaa hiyo, Renatus Mulunga, amewakabidhi  hundi ya shilingi milioni 40 kwa vikundi hivyo ambapo kila kimoja kitapata milioni mbili.

Mulunga alisema, vijana na wanawake  wanatakiwa kufanya kazi kwa bidii na kutumia fedha hizo vizuri,  ili kuweza kutatua changamoto zinazowakabili katika  biashara na miradi yao.

 “Tumewapa mkopo  wa milioni 40 mtarejesha kwa  miezi kumi na mbili  kwa asilimia 10 ya mkopo wenu, kwa ajili ya kuendeleza miradi yenu, hivyo tutawafatilia na kuhakikisha mnarejesha   kwa wakati ili na  vikundi vingine viweze kukopa, kwani manispaa hii kuna vikundi zaidi  ya 1000, katika kata zetu tunataka kila kikundi  kulichosajiliwa kipate fedha hizi na kuweza  kujikwamua kiuchumi,”alisema Mulunga.

Alisema watu wanatakiwa kuwa na juhudi ya kufanya kazi kwa bidii pamoja na kujiunga katika vikundi kwani Serikali haiwezi kugawa fedha kwa kila mtu,ambaye hajishughulishi.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Jamii, Afya na  Elimu, Sarah  Nghwani, alisema,   fedha hizo zitatolewa kwa wanawake asilimia tano na vijana tano ili wawaeze kufanya kazi kwa pamoja na kurejesha fedha hizo kwa wakati.

“Nawaomba  fedha  hizi mkazitumie vizuri   kwani siyo za luzuku tumewakopesha, mkazifanyie biashara,sambamba na kurejesha kwa wakati ili na wenzenu waweze kukopa , pia  mkawe mabalozi kwa vikundi vingine  ambavyo havijasijiliwa  viweze kujisajili na kupata mkopo kwani kuna watu wa naogopa kukopa.

No comments:

Powered by Blogger.