LIVE STREAM ADS

Header Ads

WAKILI TUNDU LISU AONDOA PINGAMIZI MAHAKAMANI KWENYE KESI YA KUPINGA MATOKEO JIMBO LA BUNDA MJINI.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Na Rose Jacob, Musoma
Wakili wa wajibu maombi wa kesi namba moja ya mwaka 2015 ya uchaguzi wa Jimbo la Bunda Mjini, Tundu Lisu, jana aliomba Mahakama kuu Tanzania inayoendelea Musoma  mkoani Mara, kufutilia mbali shauri hilo kwa madai ya ushahidi uliotolewa na upande wa waleta maombi hauna uhalali wa kumuwezesha mteja wake ambaye ni mjibu maombi namba moja Estar Bulaya kuweza kujitetea.

Hali hiyo ilijitokeza juzi kufuatia shahidi namba tatu Steven Wasira kukamilisha ushahidi na mawakili wake ambao ni Cosntantini Mtalemwa, Ajira Mungula na Yassini Membar, kuileza mahakama kuwa wamekamilisha ushahidi wao, huku lisu akieleza mahakama kuwa hatoleta shaidi kufuatia mteja wake kuonekana hana kesi ya kujibu.

Hata vivyo jana Lisu aliishangaza mahakama hiyo kwa kubadilisha uwamuzi wake na kuiomba mahakama  kesi hiyo ilendelee kusikilizwa,huku akidai kutoendelea na shauli hakutoipotzea mahakama muda,ikiwa leo atamleta shahidi namba moja kuja kutoa ushahidi ambaye ni mbunge wa jimbo la Bunda Mjini  Estar Bulaya.

“Jana (juzi) niliiomba Mahakam kufutilia mbali shauri hili kufuatia ushahidi ulioletwa na upande wa waleta maombi haujajitosheleza  kudhibitisha tuhuma zilizopo katika hati ya maombi kwa kiwango kinachotakiwa, hivyo tuliiomba Mahakama itoe ruhusa ya kutokuwepo hoja ya wajibu maombi kujitetea,lakini tumekaa tukatafakari na kushauriana tukaona tuliondoe pingamizi hilo,  hivyo kutokana na kutokamika kwa ushahidi huo hatutoacha kujibu tuhuma hizo naiomba mahakama iendelee na shauri hilo,nashadi leo ataoa ushahidi ni Estar Bulaya ,”alisema Lisu.

Aidha kwa Upande wa waleta maombi wakili Ajira Mungula aliiomba mahakama kutopokea vielezo ambayo havikuwepo tokea vilipotakiwa kupelekwa mnamo Desemba 28 mwaka jana wakati vielelezo vyote vilitakiwa kuwasilishwa kesi ilipoanza kusajiliwa na ni mwaka sasa umepita hadi kufikia hiyo jana, kufuatia Mwanasheria mkuu wa serikali Angela Lushagabala kuiomba makama ikubalinenaye kupokea vielezo vya mjibu maombi namba mbili na tatu pindi atakapo viwakilisha mahali hapo.

Aidha Jaji Noel Chocha baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili alisema, mahakama imeridhia hoja ya Lisu yakutokuwepo na hoja ya kujibu mahakamani hivyo mahakama ilmekubaliana naye kuliondoa pingamizi lake,huku akitoa maelekezo ya utetezi wa mjibu maombi Esta Bulaya utaanza leo na mjibu maombi namba mbili na namba tatu utafuata mara baada ya mjibu maombi wa kwanza kumaliza.  

Chocha alisema maamuzi ya maombi ya kuleta vielelezo vitajibiwa leo Asubuhi kabla ya kuanza kusikiliza shauri,huku akiahilisha kesi hiyo hadi 0ctoba 12 Mwaka huu.

No comments:

Powered by Blogger.