FOUNDATION KARIBU TANZANIA WATAKA UKATILI WA MAJUMBANI UTOKOMEZWE NCHINI.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Judith Ferdinand, Mwanza
Viongozi mbalimbali nchini wakiwemo wa dini na siasa wametakiwa kukemea vitendo vya ukatili majumbani wanaofanyiwa watoto, ili kukomesha na kutokomeza vitendo hivyo.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali linalojishughulisha na kupinga ukatili dhidi ya watoto majumbani Foundation Karibu Tanzania (FKT) Benard Makachia, katika mafunzo ya kupinga ukatili kwa viongozi mbalimbali, yaliyofanyika kwenye uwanja wa shirika hilo,lililipo wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza.
Makachia alisema, ili kukomesha ukatili dhidi ya watoto, viongozi mbalimbali wakiwemo wa dini na siasa kwa nafasi zao,wanatakiwa kukemea na kuelimisha jamii kupinga vitendo hivyo.
Pia alisema, jamii inapaswa kutoa taarifa kwa vyombo vya dora juu ya ukatili majumbani ili kuweza kuchukua sheria dhidi ya watu hao.
Aidha aliwaomba, wazazi na walezi kuwaelimisha watoto wao, kutambua haki na wajibu wao kwa jamii na taifa Kwa ujumla.
“Nawaomba wazazi na viongozi wa dini kutoa taarifa pindi mtakapo sikia kuna mzazi anafanya vitendo vya ukatili kwa watoto,ili kumchukulia hatua za kisheria,”alisema Makachia.
Naye Ofisa Uhusiano wa Shirika hilo Johanes Emmanuel alisema, kila mzazi anatakiwa kutoa elimu ya kupinga ukatili dhidi ya watoto sambamba na kukemea vitendo hivyo.
Kwa upande wa Mjumbe wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), wilaya ya Nyamagana Kitati Wambura na Katibu wa Jumuiya ya Wanawake BAKWATA Mkoa wa Mwanza Bi Sikitu Abubakari walisema, kuna kila haja ya jumuiya mbalimbali kupiga kelele juu ya ukatili dhidi ya watoto ili kuepuka kuwa na taifa lenye ukatili duniani.
Naye Katibu Mwenezi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema wilaya ya Ilemela Julius Malifedha alisema, ili kuepusha ukatili ni vema wanasiasa wakawa na utaratibu wa kuwakumbusha wananchi juu ya kukemea vitendo hivyo.
Judith Ferdinand, Mwanza
Viongozi mbalimbali nchini wakiwemo wa dini na siasa wametakiwa kukemea vitendo vya ukatili majumbani wanaofanyiwa watoto, ili kukomesha na kutokomeza vitendo hivyo.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali linalojishughulisha na kupinga ukatili dhidi ya watoto majumbani Foundation Karibu Tanzania (FKT) Benard Makachia, katika mafunzo ya kupinga ukatili kwa viongozi mbalimbali, yaliyofanyika kwenye uwanja wa shirika hilo,lililipo wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza.
Makachia alisema, ili kukomesha ukatili dhidi ya watoto, viongozi mbalimbali wakiwemo wa dini na siasa kwa nafasi zao,wanatakiwa kukemea na kuelimisha jamii kupinga vitendo hivyo.
Pia alisema, jamii inapaswa kutoa taarifa kwa vyombo vya dora juu ya ukatili majumbani ili kuweza kuchukua sheria dhidi ya watu hao.
Aidha aliwaomba, wazazi na walezi kuwaelimisha watoto wao, kutambua haki na wajibu wao kwa jamii na taifa Kwa ujumla.
“Nawaomba wazazi na viongozi wa dini kutoa taarifa pindi mtakapo sikia kuna mzazi anafanya vitendo vya ukatili kwa watoto,ili kumchukulia hatua za kisheria,”alisema Makachia.
Naye Ofisa Uhusiano wa Shirika hilo Johanes Emmanuel alisema, kila mzazi anatakiwa kutoa elimu ya kupinga ukatili dhidi ya watoto sambamba na kukemea vitendo hivyo.
Kwa upande wa Mjumbe wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), wilaya ya Nyamagana Kitati Wambura na Katibu wa Jumuiya ya Wanawake BAKWATA Mkoa wa Mwanza Bi Sikitu Abubakari walisema, kuna kila haja ya jumuiya mbalimbali kupiga kelele juu ya ukatili dhidi ya watoto ili kuepuka kuwa na taifa lenye ukatili duniani.
Naye Katibu Mwenezi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema wilaya ya Ilemela Julius Malifedha alisema, ili kuepusha ukatili ni vema wanasiasa wakawa na utaratibu wa kuwakumbusha wananchi juu ya kukemea vitendo hivyo.
No comments: