LIVE STREAM ADS

Header Ads

HUDUMA ZA AFYA ZIENDELEE KUBORESHWA NCHINI IKIWEMO HOSPITALI YA WILAYA TARIME MKOANI MARA.

"Nimekutana na Dr.Samwel (kushoto) katika Hospital ya Wilaya Tarime mkoani Mara, hatukuwahi kukuta hapo awali mbali ya kuchat kwenye mitandao ya kijamii (Whatsupp Groups).

Ahsante kwa Hekima zako Dr.Sammy, Jamii inakutegemea sana, hivyo hitimu vyema masomo yako ili ukaihudumie.

Nasaha za BMG ni kwamba, huduma za afya nchini bado ni Changamoto kubwa nchini kwani katika hospital, zahanati na vituo vya afya ikiwemo hospitali ya Wilaya Tarime upatikanaji wa dawa na vifaa tiba ni kilio kikubwa. Ukitaka kuelewa, uguliwa/ ugua ndipo utanielewa vyema.

Nina imani Serikali itaendelea kuboresha upatikanaji wa dawa, vitendea kazi pamoja na maslahi ya wahudumu wa afya ili kuwa ari ya kutetea afya za wananchi. Tuwaombee wagonjwa wote (akiwemo mama yangu mzazi) wapate ahueni mapema, Amen". George Binagi wa #LakeFm & #BMGHABARI

No comments:

Powered by Blogger.