NASAHA ZA BMG KUHUSU UWANJA WA NYAMAGANA JIJINI MWANZA.
BMG inasema "Ahsante kwa walionusuru hilo. Lakini pia walionusuru kuuzwa kwa uwanja huu ili ijengwe hoteli utadhani Mwanza kuna uhaba wa maeneo ya uwekezaji. Aibu!".
Licha ya kuwa na historia pana kwenye masuala ya kijamii na ukombozi wa Tanganyika, kwenye soka itakumbukwa kwamba mwaka 1974 timu za Simba na Yanga zilikutana kwenye uwanja huu kwenye Fainali ya Ligi ya Taifa ya Soka ambapo Yanga iliichapa Simba bao 2-1.
BMG tunahimiza kwamba, pamoja na wadau wengine, Kampuni ya Mafuta ya MOIL kama ilivyoahidi kupitia kwa Mkurugenzi wake, Altaf Mansoor, ipewe fursa ya kutekeleza ahadi yake ya ujenzi wa majukwaa kwenye uwanja huu mkongwe tangu mwaka 1945 ili sasa uwe na hadi yake.
'\
No comments: