LIVE STREAM ADS

Header Ads

NI UPENDO MKUBWA TAMASHA LA KIMATAIFA LA FILAMU ZANZIBAR KUFANYIKA MKOANI GEITA.

"Jumamosi wiki iliyopita nilikuwa mkoani Geita kwenye Uzinduzi wa Mradi wa Uoneshaji Filamu bure kwenye maeneo ya wazi ili kufikisha elimu mbalimbali kwa umma ikiwemo utunzaji wa mazingira, ujasiriamali pamoja na kuzuia ukatili wa kijinsia ikiwa ni miongoni mwa mambo mengi.

Mradi uko chini ya taasisi ya Kijani Consult Tanzania ya mkoani Geita kwa ufadhiri wa Zanzibar Interntional Film Festival ZIFF.
Wikendi yangu ilikuwa poa kwani pia Bodi ya Filamu Tanzania chini ya Katibu Mtendaji, Bi.Joyce Fissoo, na viongozi wengine, alikutana na Wanatasnia ya filamu mkoani Geita na kuzungumza mikakati mbalimbali ya kukuza sekta hiyo.

Jambo jema zaidi ni Tamasha la Kimataifa la Filamu Zanzibar kutangazwa pia kwamba litafanyika mwakani mkoani Geita. Ahsante Bodi ya Filamu Tanzania pamoja na ZIFF kwa upendo huo kwa wanatasnia ya filamu mkoani Geita". George Binagi #BMG & #LakeFm

No comments:

Powered by Blogger.