LIVE STREAM ADS

Header Ads

TANZIA: FAMILIA YA BINAGI ILIYOPO JIJINI DAR ES SALAA INASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA MZEE WAO, RICHARD BINAGI.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Familia ya Binagi iliyopo Kipunguni Jijini Dar es salaam, inasikitika kutangaza kifo cha mpendwa wao, Mzee Ryoba Richard Maihagya Binagi, kilichotokea leo Novemba 08,2016 asubuhi, baada ya kuugua kwa muda.

Habari ziwafikie wanafamilia wote wa Binagi waliopo mikoa mbalimbali nchini ikiwemo Dar es salaam, Mwanza na Mara pamoja na watoto wa marehemu walio nje ya nchi ikiwemo Marekani, bila kuwasahau ndugu, jamaa na marafiki.

Taratibu za mazishi zinafanyika nyumbani kwa marehemu Jijini Dar es salaam. Bwana Alitoa na Bwana Ametwaa, Jina Lake Libarikiwe, Amina!

Kumbukumbu: Marehemu Mzee Richard Maihagya Binagi alizaliwa mwaka 1928 Tarime mkoani Mara hivyo hadi mauti yanamkuta (2016), alikuwa na miaka 88 ambapo alikuwa ni askari mstaafu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).

No comments:

Powered by Blogger.