DC KINONDONI AHIMIZA WAKALA WA MISITU KUSAIDIA MBAO ZA UJENZI WA MADARASA.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Na James Salvatory, BMG Dar
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es salaam, Ally Hapi, ameiomba Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kuwasaidia mbao kwa lengo la ujenzi wa vyumba vya madarasa .
Akizungumza leo katika hafla fupi ya kukabiziwa madawati 80 yenye thamani ya shililingi milioni tano na laki sita kutoka kwa wakala wa huduma za misitu Tanzania mkuu huyo wa wilaya amesema kutokana na ongezeko kubwa la wanafunzi kwa sasa, wanaupungufu wa vyumba vya madarasa 1,068, na upungufu wa matundu ya vyoo 2,759 ,katika shule za msingi katika manispaa ya kinondondoni .
Aidha hapi amesema kuwa Raisi wa jamuhuri wa muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli aliwasaidi fedha za kujenga madarasa 22 na kwa fedha hizo wameshajenga shule mbili mpya na kuna wadau mbalimbali wameshawaidia vifaa mbalimbali vya ujenzi ikiwemo mabati,simenti na kuwaomba mbao ambazo zitaweza kujenga vyumba 1068 na kuwaomba wadau wengine wote waweze kuunga juhudi za ujenzi wa vyumba vya madarasa na vyoo vinavyoikabili wilaya ya kinondoni
Naye meneja wa wakala wa huduma za misitu Tanzania Alexander Mboya amekabizi madawati 80 yenye thamani ya shililingi milioni 5 na laki sita kwa ajiri ya shule za msingi mbili ikwemo ya msingi kigogo na Ilonda ambayo kila shule itapata madawati 40.
Na James Salvatory, BMG Dar
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es salaam, Ally Hapi, ameiomba Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kuwasaidia mbao kwa lengo la ujenzi wa vyumba vya madarasa .
Akizungumza leo katika hafla fupi ya kukabiziwa madawati 80 yenye thamani ya shililingi milioni tano na laki sita kutoka kwa wakala wa huduma za misitu Tanzania mkuu huyo wa wilaya amesema kutokana na ongezeko kubwa la wanafunzi kwa sasa, wanaupungufu wa vyumba vya madarasa 1,068, na upungufu wa matundu ya vyoo 2,759 ,katika shule za msingi katika manispaa ya kinondondoni .
Aidha hapi amesema kuwa Raisi wa jamuhuri wa muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli aliwasaidi fedha za kujenga madarasa 22 na kwa fedha hizo wameshajenga shule mbili mpya na kuna wadau mbalimbali wameshawaidia vifaa mbalimbali vya ujenzi ikiwemo mabati,simenti na kuwaomba mbao ambazo zitaweza kujenga vyumba 1068 na kuwaomba wadau wengine wote waweze kuunga juhudi za ujenzi wa vyumba vya madarasa na vyoo vinavyoikabili wilaya ya kinondoni
Naye meneja wa wakala wa huduma za misitu Tanzania Alexander Mboya amekabizi madawati 80 yenye thamani ya shililingi milioni 5 na laki sita kwa ajiri ya shule za msingi mbili ikwemo ya msingi kigogo na Ilonda ambayo kila shule itapata madawati 40.
No comments: