LIVE STREAM ADS

Header Ads

KUHUSIANA NA SAKATA LA MACHINGA JIJINI MWANZA.

Kwa  wale  wakazi  wa Jiji la  Mwanza, leo  hii  gumzo ni  kutolewa  au  kutotolewa  kwa  wamachinga, kama  jinsi  agizo  la Serikali   Jijini  Mwanza  lilivyoelekeza kuwa, mwisho ni  Disemba, 2 kwa wanachinga  kuondoka  kwenye  maeneo  yasiyo  rasmi.
Nimeguswa    na suala  hili,   hapa  kuna  pande  mbili  zinazohusika, moja  ni  Serikali  kwenye  kusimamia  agizo  lake  na pili ni  kwa wanachinga  wanaoomba  hurma  ya  Serikali  ili waendeleee  kuwepo.

Ni  wazi  Serikali   ina  dhamira  nzuri  ya  kusimamia sheria  zake  kwenye  halmashauri  hasa  kwenye  kuliweka Jii  safi na kulinda maslahi  ya  wale  wanaofanya  biashara  kihalali baada  ya kulasimisha  biashara  zako  (business  formalization)
Sheria  hizo  ni  muhimu  sana  na  zinatumika  katika  Majiji  mbalimbali  kama Nairobi, Kampala  na kwingineko, nina  imani  Serikali ya  Mkoa wa Mwanza  wanatumia mode hiyo  kwa  nia  njema.

Madai  ya  wanachinga  nayo yana  msingi wake  kuwa, wangeandaliwa  maeneo  mengine  hapa  Mjini kwa  ajili  ya biashara , nukuu  ya  kauli  ya  Rais  inatumiwa  sana, kwa  wao  kuona  wanaendelea  kufanya biashara   kwenye  maeneo  ya  mijini.

Kimsingi   kuna kila  sababu  ya  kuathirika  kiuchumi  endapo  wataenda katika  maeneo  ambayo serikali imewapangia  kwani hayajafanyiwa  upembuzi  wa awali kwenye  kubaini  manufaa/hasara za maeneo  hayo,  ndio  maana  wengi  wamekuwa  wanyenyekevu wakiiomba  serikali kufikiria  upya  uamuzi  huo.

Mtazamo wangu
Suala  la  maridhiano  ndilo  pekee  linaloweza  kusaidia  kumaliza mgogoro huu, kuliko  njia  nyingine  yoyote  ile, serikali  ikubali  kupoteza   sehemu  ya  maamuzi  yake (Mandatory  decision)  na  wamachinga  wakubali kupoteza  nusu  ya  maslahi  yao (Win – win  situation).

Najua  serikali ina  nia  njema  sana  kwenye  hili  lakini  ni  vyema  ikajaribu  kutazama  na  utetezi wa upande wa pili ili  iweze  kujenga  mahusiano  mazuri  na wananchi wake, ambao pia  ni wapiga  kura kwenye  uchaguzi ujao  wa mwaka 2020
Ebu  tuone  hili kwa  jicho  la  fundi  saa (smart thinking), na ikumbukwe  kuwa, Rais  wetu  ni  mtu  wa  wananchi  wa  kawaida  kwani  kwa  kauli  yake  ndio  waliomchagua.

Nakumbuka  wimbo  ule  wa  Tanzania  kisiwa  cha  amani  nahisi  tutaukumbuka, sidhani  kama  matumizi  ya  nguvu  yatasaidia  kumaliza  mgogoro  huu.

Namjua  mkuu  wa Mkoa wa Mwanza  kaka  yangu   John Mongella  ni  mtu  mwenye  uwezo  mkubwa  ana kila sababu  ya  kutumia  vipawa  vyake  kwenye  kuliona  jambo  hili.

“Hivi  tunashindwaje  kufunga  barabara  moja  na tukawaruhusu  watu  wetu  wakafanya  biashara  na tukakusanya  kodi” Alisema  Mh. Rais  kwenye  ziara  yake  ya  kuwashukuru  wakazi  za Mwanza  kwa kumchagua,  ipo  mifano  mingi  inayotumiwa  na  miji  mbalimbali lakini  kwa misingi  ya kutazama  faida  na hasara  ya  jambo ( cost-benefit analysis).

Aliyekuwa  Rais  wa Afrika  Kusini  Nelson Mandela  aliamini maridhiano  ndio  msingi mkubwa  wa mgogoro  wowote  ule.
Edwin Soko, Mwanahabari

No comments:

Powered by Blogger.