MWANZA WATAKIWA KUTOENDEKEZA SIASA KWENYE SHUGHULI ZA KINZENGO.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Judith Ferdinand, Mwanza
Vyama vya siasa mkoani Mwanza vimetakiwa, kuacha tabia ya kufanya shughuli za zengo (za kijamii) kisiasa.
Wito huo ulitolewa jana na Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Isamilo Kaskazini A, wilaya ya Nyamagana mkoani humo, Emmanuel Isack.
Isack alisema, wananchi ambao ni wafuasi wa vyama vya siasa wanatakiwa kuacha kuhusisha mambo ya siasa na shughuli za zengo, kwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria na taratibu.
Pia alisema, mambo ya siasa yamekwisha muda wake,muda uliopo ni wakufanya kazi na shughuli za kijamii bila ya kuhusisha itikadi za kisiasa.
Hii ni kutokana na mjumbe wa serikali za mtaa huo kupigwa na wananchi wanaosadikiwa ni wafuasi wa chama
cha siasa, waliokuwa wanataka wanazengo wa mtaa huo kutoshiriki maziko,kwenye msiba uliotokea desemba 14 mwaka huu.
"Naskitika kuona wananchi wanaleta mambo ya siasa kwenye misiba, kwani nilipata kipigo kutoka kwa wafuasi wa chama kimoja cha siasa, mara baada ya kutokea sintofahamu baina ya nzengo na wafuasi hao," alisema Isack.
Hata hivyo alisema, kama kuna msiba ni vema kuwaachia wenye msiba na siyo kuleta mambo ambayo hayahusiani na sehemu husika.
Kwa upande wa Mwenyekiti wa Mtaa huo Kombozi Kassim alisema, kitendo cha kumpiga mjumbe huyo siyo kizuri kwani kufanya hivyo ni kosa.
Aidha aliwaomba, wananchi kufanya kazi kwa bidii kwani maendeleo hayaji kwa lelemama na kuacha mambo ya siasa, ambayo muda wake umepita.
"tukiendekeza mambo ya siasa hadi msibani hatuta zikana, kuna watu wengine hawana vyama je hao watazikwa na nani?" alihoji kasimu.
Judith Ferdinand, Mwanza
Vyama vya siasa mkoani Mwanza vimetakiwa, kuacha tabia ya kufanya shughuli za zengo (za kijamii) kisiasa.
Wito huo ulitolewa jana na Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Isamilo Kaskazini A, wilaya ya Nyamagana mkoani humo, Emmanuel Isack.
Isack alisema, wananchi ambao ni wafuasi wa vyama vya siasa wanatakiwa kuacha kuhusisha mambo ya siasa na shughuli za zengo, kwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria na taratibu.
Pia alisema, mambo ya siasa yamekwisha muda wake,muda uliopo ni wakufanya kazi na shughuli za kijamii bila ya kuhusisha itikadi za kisiasa.
Hii ni kutokana na mjumbe wa serikali za mtaa huo kupigwa na wananchi wanaosadikiwa ni wafuasi wa chama
cha siasa, waliokuwa wanataka wanazengo wa mtaa huo kutoshiriki maziko,kwenye msiba uliotokea desemba 14 mwaka huu.
"Naskitika kuona wananchi wanaleta mambo ya siasa kwenye misiba, kwani nilipata kipigo kutoka kwa wafuasi wa chama kimoja cha siasa, mara baada ya kutokea sintofahamu baina ya nzengo na wafuasi hao," alisema Isack.
Hata hivyo alisema, kama kuna msiba ni vema kuwaachia wenye msiba na siyo kuleta mambo ambayo hayahusiani na sehemu husika.
Kwa upande wa Mwenyekiti wa Mtaa huo Kombozi Kassim alisema, kitendo cha kumpiga mjumbe huyo siyo kizuri kwani kufanya hivyo ni kosa.
Aidha aliwaomba, wananchi kufanya kazi kwa bidii kwani maendeleo hayaji kwa lelemama na kuacha mambo ya siasa, ambayo muda wake umepita.
"tukiendekeza mambo ya siasa hadi msibani hatuta zikana, kuna watu wengine hawana vyama je hao watazikwa na nani?" alihoji kasimu.
No comments: