LIVE STREAM ADS

Header Ads

WATUMISHI WA MUNGU NCHINI WAASWA KUWASAIDIA WENYE UHITAJI.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com


 Nabii mkuu mheshimiwa Dr.Geordavie akiombea  bajeti mbalimbali  za waumini walizozileta kwa ajili ya kutolewa neno la unabii, siku ya jana
Nabii mkuu mheshimiwa Dr Geordavie akiwa anahubiri katika
hema la kukutania ngurumo ya upako kisongo jijini Arusha
 Nabii mkuu akiwa anaendelea na huduma  ya sikuu kuu 
Nabii akiwa anamwaga upako kwa waumi waliohudhuria

Na woinde Shizza,Arusha
Watumishi wa Mungu na waumini wa madhehebu mbalimbali ya dini nchini wametakiwa kujijengea tabia ya kuwasaidia wenye uhitaji wakiwemo yatima ili nao waweze kujisikia kama ni sehemu ya jamii.

Hayo yalibainishwa jana na Nabii mkuu mheshimiwa Dr.Geordavie wakati akifanya  dua maalumu ya kupitisha bajeti ya watu walioshiriki katika sikukuu ya kukusanya iliyofanyika katika hema la kukutania ngurumo ya upako kisongo jijini Arusha.

Alisema kuwa ni wajibu wa kila mtumishi kukusanya  na kutoa kile alichonauwezo nacho ili  kuweza kuwasaidia watoto yatima ,wananchi wasiojiweza  ili kuweza kuwafanya nao wajisikie ni sehemu ya jamii

Alisema kuwa mbali na watoto yatima pia aliwasihi makanisa ambayo yanajiweza kuweza kusaidia yale ambayo ni machanga ili kuweza kuwapa nguvu ya kuweza kuendelea kueneza injili na kumtangaza mungu  kupitia makanisa yao.

Nabii mkuu Dr Geordavie alisema kuwa  kuwa lengo la sikukuu hii ya kukusanya nikuwasaidia watoto yatima kwa kuwapa chakula kama mchele, sukari pamoja na mafuta yakupikia ili nao wajisikie wanafuraha haswa katika kipindi hichi cha sikukuu.

Alisema kuwa  licha ya misaada hiyo kwenda kwa watoto yatima, pia atatoa fedha kwa watumishi wa mungu wenye makanisa madogo hapa nchini lengo likiwa ni kuinua huduma zao na kuwasaidia katika kuendeleza huduma zao ikiwa ni pamoja na ujenzi wa kanisa, ununuzi wa vyombo vya muziki na shughuli nyingine za kanisa.

Sikukuu hii ya kukusanya  huadhimishwa na huduma ya Ngurumo ya Upako Duniani tarehe 26 ya kila mwaka, watu hutoa sadaka ya vitu mbalimbali ikiwemo fedha kwa mujibu wa maelekezo ya Nabii Mkuu na kisha hugawanywa kwa vituo vya watoto yatima  huku  fedha zikigawanywa kwa watumishi waliotuma maombi ya kupata msaada   wa kuendeleza huduma zao.

Mwaka jana msaada wa zaidi ya shilingi milioni 15 ulitolewa na waumini wa kanisa la Ngurumo ya upako na kugawanywa katika vituo mbalimbali vya watoto yatima huku fedha zikigawiwa kwa baadhi ya makanisa madogo  kwa ajili ya kuwasaidia mambo mbalimbali.

No comments:

Powered by Blogger.