LIVE STREAM ADS

Header Ads

MASHINDANO YA LIGI DARAJA LA NNE NGAZI YA WILAYA YA GEITA YAFUNGULIWA RASMI.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Timu ya Bukoli FC wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya mchezo kuanza

Timu ya Bomani kutoka mjini Geita wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya mchezo kuanza.

Kaimu Mgeni Rasmi ambaye ni Diwani wa Bukoli  Faraji Seif  akikagua vikosi na kusalimiana na wachezaji wa timu zote mbili yaani Bukoli Fc na Bomani 

Mgeni Rasmi akiongozwa na kapteni wa timu ya Bukoli Fc akisalimiana na wachezaji wa timu hiyo kabla ya mchezo kuanza.

Mh,Faraji Seif ambaye ndiye mgeni rasimi kwenye uzinduzi wa ligi daraja la nne wilaya ya Geita akifatilia kwa makini mchezo uliokuwa ukiendelea uwanjani

Mlinda mlango wa timu ya Bomani akitoka nje baada ya kuwa amepata majeraha katika mchezo huo.

Mlinda mlango akiwa amebebwa .

Baadhi ya mashabiki wakiendelea kufatilia kwa umakini mechi ambayo ilikuwa inaendelea uwanjani.

Mashambulizi yakiendelea kwa kasi kubwa kwenye viwanja vya bukoli





Mwamuzi wa mchezo huo , Majeshi Mgema akitoa maelekezo kwa wachezaji wa timu ya Bomani.
MADUKAONLINE
Mashindano ya Soka Ligi daraja la nne (4) ngazi ya wilaya ya Geita yameanza kutimua Vumbi jana ambapo Mechi ya Ufunguzi ilikuwa kati ya Bukoli FC dhidi ya  Bomani FC na Mshindi ameibuka Bukoli kwa goli tatu(3)didi ya Bomani kutoka mjini Geita.

 Ilikiuwa siku ya  jana January 19,2017 majira ya jioni ambao Historia imeandikwa kwa mala ya kwanza baada ya miaka ishiriki ( 20)kupatikana kwa kituo cha ufunguzi wa Ligi daraja la nne ngazi ya wilaya.

Akifungua mashindano hayo kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Geita Mwl,Herman Kapufi ambaye alitarajia kuwa mgeni rasmi Diwani wa Kata ya Bukoli Faraji Seif,aliwataka wachezaji kuwa na nidhamu ya hali ya juu katika kipindi chote cha ligi huku akiwataka mashabiki kuwa na nidhamu katika swala la ushangiliaji.

“Natambua kuwa michezo ni ajira ni vyema kutumia nafasi hii kwa kujituma kwa timu zote ambazo zitashiriki ligi hii na niwaombe sana wale ambao mtashindwa mkubali kushindwa maana mchezo ni dakika sitini(90) kwa hiyo hatutarajii kuona mnakuwa sio watu wa kuheshimiana jambo la msingi wasikilizeni walimu wenu nikiwa na maana makocha na pia muwe watu wa kujituma kwenye mazoezi naamini mkizingatia haya basi mtafanya vizuri timu zote”aliwasisitiza Seif

Katika mechi ya ufunguzi wenyeji Bukoli waliitandika    Boman FC mikwaju mitatu dhidi ya miwili katika kipindi cha pili .katika mchezo huo uliochezeshwa na mwamuzi Majeshi Mgema.

Mabadiliko makubwa yalionekana katika kipindi cha pili ambapo timu zote zilionesha ushindani na kucheza kwa kukamiana ambapo kunako dakika ya hamsini(50) mchezaji Shukuru Mtesiga aliiandikia bao la kwanza Bukoli FC, na dakika ya  hamsini na saba (57) mchezaji mwenzake Marius Joseph akafunga goli la pili

Bomani FC wakapata goli la kwanza katika dakika ya sitini na saba ( 67 )kupitia kwa mchezaji wao Kasaba Sabu,na dakika ya sabini na saba (77)kwa mara nyingine Shukuru Mutesiga aliyeonekana kinara katika mchezo huo akaipatia ushindi timu ya Bukoli kwakuzamisha mpira kimiani na kuandika bao la  tatu(3). Goli la pili la Bomani lilipatikana kunako dakika ya themanini na mbili (82 )kupitia kwa mchezaji John Pastory.

No comments:

Powered by Blogger.