LIVE STREAM ADS

Header Ads

TAASISI YA AGRI-BUSNESS MEDIA INITIATIVE YA JIJINI MWANZA YAWAHIMIZA VIJANA KUJIKITA KWENYE KILIMO.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Mkurugenzi wa Taasisi ya Agri-Busness Media Initiative In Tanzania (AMI-TZ) ya Jijini Mwanza, Deborah Mallaba, akikagua shamba la hekari mbili la taasisi hiyo ambalo lina mkusanyiko wa matunda na mbogamboga za aina mbalimbali, lililopo Igombe Ziwani, Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza.

Na Binagi Media Group
Taasisi ya AMI-TZ inajihusika na kilimo cha matunda na mbogamboga kama vile matikiti maji, nyanya, bamia, nyanya, pilipili mbuzi na aina nyinginezo nyingi.

Baada ya mavuno, taasisi hiyo hufanya usindikaji wa mazao kwa ajili ya kuwafikishia wateja wake majumbani, maofisini na mengine huuzwa moja kwa moja shambani.

"Baadhi ya vijana ukiwaeleza suala la kilimo wanakuona kama vile umepitwa na wakati lakini wale wanaojitambua wameingia kwenye kilimo na kinawalipa. Hivyo niwahamasishe watumie muda wao vizuri kwa kujishughulisha kwenye kilimo hivyo wasisubiri tu kazi za maofisini". Anasisitiza Deborah Mallaba, Mwanahabari na Mkurugenzi wa Taasisi ya AMI-TZ.

Mallaba anawasisitiza viongozi wa serikali kuanzia ngazi ya Kata hadi Wilaya, kuongeza jitihasa za kuwakusanya vijana pamoja na kuwapatia mitaji ikiwemo pembejeo ili wajikite kwenye kilimo maana kilimo ni biashara na kinalipa ambapo pia hatua hio itasaidia kupunguza vijana mitaani.

"Napenda kuwaambia akina dada waamuke maana si vyema kuzurura tu wakisema hakuna ajira. Mfano mimi nimeanza kujiwekea kipato changu kupitia kilimo na nataka kuwa mafano bora kwa vijana wengine". Anasisitiza Aneth Shosha ambaye ni Afisa Masoko wa taasisi ya AMI-TZ huku akiwakaribisha vijana wengine kwenye taasisi hiyo ili wajifunze zaidi kuhusu kilimo.
Umwagiliaji kwenye shamba la bamia, kilimo hiki kinategemea maji kutoka ziwa victoria hivyo kinafanyika msimu wowote kwa mwaka.
Aneth Shosha ambaye ni Mratibu/ Afisa Masoko wa Taasisi ya Agri-Busness Media Initiative In Tanzania (AMI-TZ), akimwagilia maji kwenye shamba la bamia
Ukaguzi wa mbogamboga kila siku ni kanuni ambayo husaidia kutambua mmea unaoanza kushambuliwa na wadudu ili kwahi umwagiliaji wa dawa hususani dawa asilia
Wachapa kazi wakichakarika
Umwagiliaji wa kwenye kilimo cha nyanya
Kilimo cha matikiti maji
Kilimo cha nyanya
Kilimo cha bambia
Mfumo wa umwagiliaji kwa kutumia mashine kutoka Ziwa Victoria ndio hutumika kwenye shamba hili. 
Kwa msaada na ushauri, piga simu nambari 0754 99 66 13

No comments:

Powered by Blogger.