LIVE STREAM ADS

Header Ads

UCHAGUZI CHADEMA KANDA YA ZIWA WAONDOKA NA MWENYEKITI WA WILAYA.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Kuhusu kuhama Chama cha Siasa na kuendelea kufanya siasa bila Chama na Shilogela.

Mimi Shilogela Babila Nganga, Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Kwimba najiuhuzulu Umwenyekiti wa Chama na kuachana na Chadema na kuendelea kuwa mwanasiasa asie na Chama hadi pale nitakapo amua na kukusudia vinginevyo kwa sababu ya kutokuwa na Demokrasia katika Chama hiki, 

kama nilivyo shuhudia leo (jana) kwenye uchaguzi wa mwenyekiti kanda ya Ziwa Victoria, kwa jina langu kuenguliwa bila sababu ni sawa sawa kama alivyo wahi kuenguliwa Mh.Lowassa na CCM! na hatimae kuhamia CHADEMA ambako na sisi tunakuhama! 

Wito wangu kwa viongozi wengine wa Chama, ikiwa demokrasia na iwe hivyo kwa kuzingatia na kufuata misingi ya demokrasia na wala sio kusema Busara ya kamati kuu ya CHADEMA kufanya kazi kwa niaba ya misingi mikuu ya demokrasia na katiba ya Chama husika bila kuitii wanasiasa wa nchi hii tutakuwa tuna hamia kutoka huku na kwenda kujiunga kule, 

hivyo niko katika mawazo mtanziko na kutenga muda wa kutosha ilikutoa Maamuzi ya kisayansi nyeye afya kamili ili ni weze kuendelea kuifanya Siasa kwa sababu siweze kujitenga nayo kwani Siasa na maisha ya watu, maisha ya watu na Siasa na hakuna Siasa hakuna maisha. Soma hapa kuhusu uchaguzi

No comments:

Powered by Blogger.