HILI NDILO JIJI LA MWANZA WAKATI WA MVUA.
Pichani ni moja ya barabara za Jijini Mwanza baada ya mvua
kunyesha jana. Ilikuwa ni kero kubwa kwa watumiaji wa barabara hiyo inayotoka
Soko Kuu.
Uzoefu unaonesha kwamba mitaro kujaa uchafu husababisha kero
hiyo wakati wa mvua.
Bado kuna lawama kwa baadhi ya wanaofanya biashara katika
maduka yaliyo kwenye barabara za Jijini Mwanza kwamba wamekuwa wakitupa uchafu
katika barabara hizo na kusababisha kuziba mara kwa mara huku lawama nyingine
zikiwaendea baadhi ya wanaofanya usafi kwa kufagia uchafu kuelekea kwenye
mitaro hiyo.
Halmashauri ya Jiji la Mwanza inapaswa kuliona hili kama
tatizo na kuja na mbinu mbadala ikiwemo faini kali kwa atakayekutwa akitupa
ovyo uchafu.
#BMGHabari
No comments: