MWANZA WAHIMIZWA KUSOMESHA WATOTO WA KIKE.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Judith Ferdinand,Mwanza
Jamii mkoani Mwanza imeshauriwa kuwathamini na kuwapeleka shule watoto wa kike, ili kuweza kujikwamua kiuchumi sambamba na kuwakinga na mimba za utotoni ambazo hukatisha ndoto zao.
Ushauri huo ulitolewa jana na Mkurugenzi wa Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Education for Better and Living (EBLI) Bernard Makachia, wakati akizungumza na wanahabari Jijini Mwanza kuhusu hatua mbalimbali zinazochukuliwa na taasisi hiyo katika kuwasaidia watoto wa kike.
Makachia alisema ili kuweza kupunguza mimba za utotoni ni lazima wazazi na walezi kukemea vitendo vya ukatili kwa watoto wa kike na kuhakikisha wanawapeleka shule ili kupata elimu ambayo ndiyo urithi muhimu kwa maisha ya baadae.
“Lengo la kuanzisha kituo hiki ni kuwasaidia watoto waliokatishwa masomo wakiwa bado wadogo kwani sisi tunawafundisha ujasiriamali, masomo ya tehama na biashara, ili waweze kujiajiri wenyewe na kuepuka kuwa tegemezi,” alisema Makachia.
Pia alisema, wananuia kutoa semina kwa jamii na wanafunzi,wakishirikiana na serikali, ili kutokomeza vitendo vya ukatili kwa watoto wa kike, kwa kufanya hivyo kutasaidia kutimiza ndoto zao ambazo hukatishwa na wazazi kwa kuwathamini wakiume kulioko wao.
“Mimba za utotoni hazisababishwi na wanafunzi pekee yao bali hata kitendo cha wazazi kufumbia macho uovu huo na kuacha kuuripoti kwenye vyombo vya dola nako huchangia tatizo hili kukua, ni vyema tukaungana sote na kutokomeza vitendo hivyo,” alisema Makachia.
Taasisi ya Education for Better and living (EBLI) imejikita katika kuwasaidia watoto wa kike waliopata mimba za utotoni kwa kuwapa elimu ya ujasiliamali, biashara na tehama ili kuhakikisha wanatimiza ndoto zao za kupata elimu.
Judith Ferdinand,Mwanza
Jamii mkoani Mwanza imeshauriwa kuwathamini na kuwapeleka shule watoto wa kike, ili kuweza kujikwamua kiuchumi sambamba na kuwakinga na mimba za utotoni ambazo hukatisha ndoto zao.
Ushauri huo ulitolewa jana na Mkurugenzi wa Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Education for Better and Living (EBLI) Bernard Makachia, wakati akizungumza na wanahabari Jijini Mwanza kuhusu hatua mbalimbali zinazochukuliwa na taasisi hiyo katika kuwasaidia watoto wa kike.
Makachia alisema ili kuweza kupunguza mimba za utotoni ni lazima wazazi na walezi kukemea vitendo vya ukatili kwa watoto wa kike na kuhakikisha wanawapeleka shule ili kupata elimu ambayo ndiyo urithi muhimu kwa maisha ya baadae.
“Lengo la kuanzisha kituo hiki ni kuwasaidia watoto waliokatishwa masomo wakiwa bado wadogo kwani sisi tunawafundisha ujasiriamali, masomo ya tehama na biashara, ili waweze kujiajiri wenyewe na kuepuka kuwa tegemezi,” alisema Makachia.
Pia alisema, wananuia kutoa semina kwa jamii na wanafunzi,wakishirikiana na serikali, ili kutokomeza vitendo vya ukatili kwa watoto wa kike, kwa kufanya hivyo kutasaidia kutimiza ndoto zao ambazo hukatishwa na wazazi kwa kuwathamini wakiume kulioko wao.
“Mimba za utotoni hazisababishwi na wanafunzi pekee yao bali hata kitendo cha wazazi kufumbia macho uovu huo na kuacha kuuripoti kwenye vyombo vya dola nako huchangia tatizo hili kukua, ni vyema tukaungana sote na kutokomeza vitendo hivyo,” alisema Makachia.
Taasisi ya Education for Better and living (EBLI) imejikita katika kuwasaidia watoto wa kike waliopata mimba za utotoni kwa kuwapa elimu ya ujasiliamali, biashara na tehama ili kuhakikisha wanatimiza ndoto zao za kupata elimu.
No comments: