LIVE STREAM ADS

Header Ads

TAASISI YA METDO TANZANIA YA JIJINI MWANZA YAWASHAURI WAKULIMA KUBADILI MFUNO WAO WA KILIMO.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Mkurugenzi wa Taasisi ya Metdo Tanzania, Ashraf Omary (kulia), akizungumza na mwanahabari wa Lake Fm Mwanza, George Binagi-GB Pazzo.

#LakeFmHabari
Wakulima mkoani Mwanza wameshauriwa kubadili mfumo wa kilimo kwa kuachana na kilimo cha kutegemea mvua na badala yake wajikite kwenye kilimo cha umwagiliaji ambacho kina tija zaidi.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Metdo Tanzania ya Jijini Mwanza inayoshughulisha na utoaji wa elimu ya mazingira katika maeneo ya migodini, Ashraf Omar, alitoa ushauri huo jana wakati akizungumza na Lake Fm.

Alisema kwa idhini ya Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella, taasisi hiyo imepewa ridhaa ya kufanya tafiti za kilimo na kutoa elimu katika jamii juu ya kilimo cha umwagiliaji hivyo wakulima wanapaswa kuitumia ipasavyo ili kuboresha shughuli zao.

Tayari taasisi ya Metdo Tanzania imeanza kufanya tafiti za kilimo cha umwagiliaji katika halmashauri ya wilaya ya misungwi katika eneo la Mbalika ambako mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Eliud Mwaiteleke, anahimiza kilimo cha umwagiliaji kufanyika kwa manufaa ya jamii hususani akina mama na vijana.

No comments:

Powered by Blogger.