MAFUNDI WENYE ULEMAVU MKOANI MWANZA WAILILIA SERIKALI.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Judith Ferdinand, Mwanza
Mafundi wenye ulemavu mkoani Mwanza wameiomba serikali kuwapa mikopo ili waweze kujiendesha katika shughuli zao za kiuchumi na kuacha kuwa ombanba sambamba na tegemezi kwenye familia.
Hayo yalisenwa jana na mafundi wa Karakana ya Nyakato Tri-cyle Work Shop iliyopo wilayani Ilemela mkoani Mwanza wakati wakizungumza na BMG.
Mmoja wa mafundi hao John Kerenge alisema, serikali ikiwawezesha Walemavu kwa kuwapa mikopo, ili waweze kujiingizia kipato kupitia ujuzi walionao itasaidia kupunguza ombaomba na tegemezi kuanzia ngazi ya familia.
“Nasikitika kuona watu wanakaa barabarani kwa lengo la kuomba, kufanya hivyo siyo vizuri kwani kuna kazi nyingi ambazo watu wenye ulemavu wanaweza kufanya na kujipatia kipato,haipendezi kuwategemezi kwa watu,”alisema Kerenge.
Pia aliiomba serikali, kuwapatia tenda pindi itakapo kuwa na kazi za kutengeneza madawati, madirisha, meza za kuchomelea, ili wajipatie kipato kwani wakiwezeshwa wanaweza.
Kwa upande wa fundi wa kalakana hiyo Veronica Mtiro alisema, serikali imewasahau katika kuwapa mikopo kwani mtaji walionao ni mdogo, hali inayosababisha kushindwa kukamilisha kazi kwa wakati pale wanapopata tena.
“Tunaiomba serikali itukumbuke na sisi, kwa kutupa mikopo kwani tuna mtaji kidogo ambao unashindwa kukidhi matakwa,pindi tunapota wateja wengi kwa wakati mmoja,"alisema Mtiro.
Hata hivyo Mabulla Erest alisema , kalakana hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo masoko na mtaji kwani kuchangia kukwamisha maendeleo ya shughuli zao.
Judith Ferdinand, Mwanza
Mafundi wenye ulemavu mkoani Mwanza wameiomba serikali kuwapa mikopo ili waweze kujiendesha katika shughuli zao za kiuchumi na kuacha kuwa ombanba sambamba na tegemezi kwenye familia.
Hayo yalisenwa jana na mafundi wa Karakana ya Nyakato Tri-cyle Work Shop iliyopo wilayani Ilemela mkoani Mwanza wakati wakizungumza na BMG.
Mmoja wa mafundi hao John Kerenge alisema, serikali ikiwawezesha Walemavu kwa kuwapa mikopo, ili waweze kujiingizia kipato kupitia ujuzi walionao itasaidia kupunguza ombaomba na tegemezi kuanzia ngazi ya familia.
“Nasikitika kuona watu wanakaa barabarani kwa lengo la kuomba, kufanya hivyo siyo vizuri kwani kuna kazi nyingi ambazo watu wenye ulemavu wanaweza kufanya na kujipatia kipato,haipendezi kuwategemezi kwa watu,”alisema Kerenge.
Pia aliiomba serikali, kuwapatia tenda pindi itakapo kuwa na kazi za kutengeneza madawati, madirisha, meza za kuchomelea, ili wajipatie kipato kwani wakiwezeshwa wanaweza.
Kwa upande wa fundi wa kalakana hiyo Veronica Mtiro alisema, serikali imewasahau katika kuwapa mikopo kwani mtaji walionao ni mdogo, hali inayosababisha kushindwa kukamilisha kazi kwa wakati pale wanapopata tena.
“Tunaiomba serikali itukumbuke na sisi, kwa kutupa mikopo kwani tuna mtaji kidogo ambao unashindwa kukidhi matakwa,pindi tunapota wateja wengi kwa wakati mmoja,"alisema Mtiro.
Hata hivyo Mabulla Erest alisema , kalakana hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo masoko na mtaji kwani kuchangia kukwamisha maendeleo ya shughuli zao.
No comments: