LIVE STREAM ADS

Header Ads

UTPC YANG'AKA SAKATA LA MAKONDA KUVAMIA CLOUDS TV AKIWA NA BUNDUKI.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Image may contain: 3 people, people sitting and outdoorJudith Ferdinand, Mwanza
Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari nchini (UTPC), umelaani kitendo kilichofanywa na kuu wa mkoa  Dar es salaam Paul Makonda cha kuingia studio za runinga cha Clouds wikendi iliyopita.

Hayo yamesemwa leo na Rais wa  UTPC, Deogratias Nsokolo (kushoto), wakati akizungumza na wanahabari katika ofisi ya umoja huo Jijini Mwanza.

"Kitendo cha kiongozi wa serikali kuvamia chombo cha habari akiambatana na askari wenye silaha, ni jambo baya sana,hivyo sisi waandishi wa habari  na wadau wetu, lazima tukilaani kwa nguvu zetu,kwani tukio kama hili halijawai kutokea nchini, " alisema Nsokolo.

Nsokolo amesema, mtu yoyote anayetaka kulazimisha habari gani itoke au isitoke,anakua anafinya uhuru wa habari, kwani kazi ya uandishi ina miiko ambayo ndio inatumika kuchagua habari ya ipi itumike ipi isitumike.

Pia amesema, ni wajibu wa waandishi wa habari na wadau wanaopenda maendeleo, kuulinda uhuru wa habari  kwa faida ya nchi, sambamba na kutoa pole kwa wamiliki na wafanyakazi wa  clouds kwa kuwatia moyo wa kuendelea na kazi ya kujenga taifa.

Hata hivyo ametoa wito kwa wadau,viongozi wa kisiasa na kiserikali kuviheshimu vyombo vya habari  na wavisaidie ili vitimize wajibu wao bila vikwazo.
Image may contain: 2 people, people sitting, table and outdoor
Kwa upande wake Mkurugenzi wa UTPC, Abubakar Karsan (kulia), amesema mwandishi kuandika habari akiwa amesimamiwa na magwanda ya kijeshi siyo vionjo vya habari, pia nchi imevunja rekodi ya mkuu wa mkoa kuingia studio za chombo cha habari.
Image may contain: 3 people, people sitting, outdoor and indoor

No comments:

Powered by Blogger.