LIVE STREAM ADS

Header Ads

WAFANYAKAZI WA SSRA WALIVYOSHIRIKI SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI (MAY DAY) JIJINI DAR ES SALAAM.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), wakiwa tayari kwa maandamano ya wafanyakazi katika kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Dei) nje ya jengo la Ofisi za Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.(Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), wakipiga picha ya pamoja kabla ya kuanza kushiriki kwenya maandamano ya wafanyakazi katika kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Dei) nje ya jengo la Ofisi za Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), wakipatiwa maelezo ya ratiba ya maandamano ya wafanyakazi katika kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Dei) na Ofisa Habari wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), wakijipanga tayari kwa kuanza kushiriki kwenya maandamano ya wafanyakazi katika kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Dei) nje ya jengo la Ofisi za Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta), Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Bendi ya Jeshi la Magereza ikiongoza maandamano ya wafanyakazi katika kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Dei) kwenye Barabara ya Nkuruma kuelekea Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), wakiwa kwenya maandamano ya wafanyakazi katika kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Dei) kwenye Barabara ya Chang'ombe jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA),wakiwa wamechanganyika na baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi nyingine kwenya maandamano ya wafanyakazi katika kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Dei) jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), wakiwa kwenya maandamano ya wafanyakazi katika kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Dei) kwenye Barabara ya Mandela, nje ya Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), wakielekezana jambo wakati wa maandamano ya wafanyakazi katika kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Dei) kwenye Barabara ya Mandela, nje ya Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam kabla ya kuingia uwanjani humo.
Bendi ya Jeshi la Magereza ikiwaongoza wafanyakazi kuingia ndani ya Uwanja wa Uhuru kwa maandamano katika kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Dei) kwenye Barabara ya Nkuruma kuelekea Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), wakipita kuelekea aliposimama mgeni rasmi, Rais mstaafu wa Chama cha Walimu (CWT), Mama Magreth Sitta ndani ya Uwanja wa Uhuru wakati wa maandamano ya wafanyakazi katika kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Dei),  jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi waMamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), wakiwa na bango lao, wakipita mbele ya mgeni rasmi, Rais mstaafu wa Chama cha Walimu (CWT), Mama Magreth Sitta ndani ya Uwanja wa Uhuru wakati wa maandamano ya wafanyakazi katika kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Dei),  jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi, Rais mstaafu wa Chama cha Walimu (CWT), Mama Magreth Sitta (katikati) akipunga mkono kuyapokea maandamano ya wafanyakazi katika kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Dei),  jijini Dar es Salaam.

No comments:

Powered by Blogger.