LIVE STREAM ADS

Header Ads

MABATINI STAR YAENDELEA KUTOA DOZI NDONDO CUP 2017 JIJINI MWANZA

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Judith Ferdinand, Mwanza
Timu ya Mabatini Star yaendelea kutoa kichapo baada ya kuifunga Nyegezi Terminal goli 3-2, katika mashindano ya Ndondo Cup yanayoendelea kutimua vumbi  kwenye uwanja wa kisasa na mkongwe wa Nyamagana jijini hapa.

Katika mchezo huo ambao ni wa raundi ya pili hatua ya makundi ilizikutanisha timu za kundi B, ambapo kipindi cha kwanza kila timu ilijitahidi kushambulia lakini juhudi hizo hazikuzaa matunda mpaka mapumziko matokeo yalikua bila bila.

Katika kipindi cha pili timu zote zilifanikiwa kutikisa nyavu za  mwenzie ambapo Mabatini Star ilifunga magoli 3 kupitia mshambuliaji wake Kanichi Andrew dakika ya 47,54 na 65 huku Nyegezi Terminal wakipata goli dakika ya 53 kupitia mshambuliaji wake Ramadhani Mandinda na  Twalibu Ally aliyefunga dakika ya 76.

Hata hivyo Kanichi Andrew ndiye aliyeibuka mchezaji bora wa mchezo huo na kufanikiwa kupatiwa zawadi ya shilingi 30000 kutoka kwa   Hasafu Barber Shop  kupitia Mkurugenzi wake Hamis Swahibu ambae amekua akiendelea kutoa zawadi kwa ajili ya kuwahamasisha wachezaji kufanya vizuri.

Kanichi alisema, siri ya ushindi ni  kujituma,mazoezi,kufuata maelekezo ya kocha,uwezo na jitihada binafsi za wachezaji.

Naye Kocha wa Mabatini Star  Omar Bakar alisema,mechi ilikua ngumu ila wanamshukuru Mungu wameweza kuibuka na ushindi.

Kwa upande wake Kocha wa Nyegezi Terminal Ibrahim Mlumba alisema, mechi ilikua ngumu,na sababu ya kupoteza mchezo huo ni kutokana na mabeki wa timu hiyo kutokua makini,hivyo wanajipanga ili mchezo ujao waweze kufanya vizuri.

Aidha timu zote mbili katika raundi ya kwanza ya hatua ya makundi ya mashindano hayo ziliweza kushinda ambapo Nyegezi Terminal ilishinda goli 1-0 dhidi ya Buzuruga Terminal huku Mabatini Star ikifunga goli 6 -3 dhidi ya Igoma Heroes.

Wakati huo huo  katika mchezo wa kwanza timu ya Iseni Fc iliibuka na ushindi wa goli 3-2 dhidi ya  Viva Fc.

Timu ya Iseni Fc ilifunga magoli kupitia washambuliaji wake Khatibu Abdallah dakika ya 2, Paul Godfrey dakika ya 61 na Juma Salige dakika ya 80, huku VIVa Fc wakifunga kupitia Ballo Kashind dakika ya 33 na Emma Kijeshi dakika ya 46.


Juma Salige ndiye aliibuka mchezaji bora katika mchezo huo na kupatiwa kitita cha shilingi 30000.

No comments:

Powered by Blogger.