Serikali yakusanya Milioni 200 baada ya ng'ombe kutoka nchi jirani kupigwa mnada wilayani Mwanga
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Waziri wa
Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina (katikati) akiongea na waandishi wa habari kuhusu
opareshei ondoa Mifugo leo katika ofisi za wizara hiyo jijini Dar es
Salaam.
Pembeni yake ni Naibu Waziri Abdalah Ulega, kulia ni Katibu Mkuu wa
Wizara hiyo katika sekta ya Mifugo Dkt Maria Mashingo na kushoto ni Katibu Mkuu
sekta ya Uvuvi Dkt. Yohana Budeba.
Evelyn Mkokoi
Kupitia amri
ya mahakama iliyoamuru kupigwa mnada kwa ng’ombe waliovamia kutoka nchi jirani ya
Kenya, Serikali imekusanya zaidi ya Shilingi Milioni 200 baada ya ng’ombe hao
kupigwa mnada katika wilaya ya Mwanga mwishoni mwa wiki.
Akiongea na
waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.
Luhaga Mpiga amesema Wizara yake imejipanga na kuendelea na Oparesheni maalum
ya kukamata na kuondoa mifugo yote inayovamia
kutoka nchi jirani kupitia mikoa ya mipakani kama Katavi, Kigoma, Tanga,
Mara,Ruvuma, na Arusha na kuagiza wakuu wa Mikoa na Wilaya hizo kuendesha
Opresheni hizo Maalum ndani ya siku saba.
“Mimi ,
Naibu Waziri wangu, makatibu wakuu na wataalam tunaingia tena katika opareshi
hiyo maalum kesho.” Alisisitiza Mpina
Aidha, Mpina
alisema kuwa serikali haipo tayari kuingia gharama ya kutibu magonjwa
yanayoletwa na mifugo wanaovamia kutoka nchi jirani ambao kwa namna moja au
nyingine huleta uharibifu wa mazingira kwa kukata miti ovyo, kusababisha
mmomonyoko wa udongo na kuchangia kwa kiasi kikubwa migogoro ya wakulima na
wafugaji.
Mpina
alisema, watu wenye nia mbaya wasihusishe Opareni hii na mahusiano ya nchi hizi
mbili akitolea mfano mahusiano ya Kenya na Tanzania katika Jumuiya ya Afrika
Mashariki kuwa yapo kisheria.
Akizungumzia
suala ya mifugo ya Tanzania kuwa na chapa Mpina alisema, suala hili
linashughulikiwa na ifikapo December mwaka huu litakuwa limekamilika na hivyo
kurahisha oparesheni hizi za kuondoa mifugo vamizi.
No comments: