LIVE STREAM ADS

Header Ads

Kampeni ya "Amsha Viwanda" yazinduliwa Nyamagana

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Msimamizi Mkuu wa  Shirika la Voluntary Service Overseas (VSO), Frank Girabi akizungumza katika uzinduzi wa kampeni ya amsha viwanda.
 Judith Ferdinand, Mwanza
Katika kuunga ndoto za Rais za kuwa na uchumi wa viwanda na  kuhakikisha  wajasiriamali wanaendelea, Shirika la Voluntary  Service Overseas (VSO) kupitia mradi wake wa  Kuwasaidia na kuendeleza Wajasiriamali Tanzania (TLED) limeanzisha  kampeni ya Amsha Viwanda.

 Kampeni hiyo ambayo itafanyika katika wilaya nne za mkoa wa Mwanza ikiwemo Nyamagana, Ilemela, Magu na Kwimba, ambayo imelenga kuhakikisha wajasiriamali wanafanya shughuli zao kwa uangalizi sambamba na kuunganishwa na wadau mbalimbali ikiwemo taasisi za kifedha na za serikali, kwa ajili ya kukuza biashara zao.

Akizungumza jana katika uzinduzi wa kampeni hiyo uliofanyika wilayani Nyamagana, Msimamizi Mkuu     mradi wa  TLED  wa  shirika la VSO Frank Girabi alisema,   kampeni hiyo ni  sehemu ya kutekeleza mradi wao ambao unafanyika kwa miaka mitano katika mikoa sita nchini ikiwemo Mwanza, wakishirikiana na SIDO,TCCIA,TWCC na ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Girabi alisema,  wamejikita katika kutoa  mafunzo na ushauri,kwani wanawasaidia wajasiriamali wadogo katika nyanja tofauti tofauti ambazo wanazokutana  na changamoto mbalimbali ikiwemo soko,usimamizi wa fedha na biashara zao.

Pia alisema, kupitia mradi huo wanatarajia kuwafikia wajasiriamali 1760 nchi nzima, hasa wakina mama ambao wanatoka katika maeneo wanawasaidia kwa kuwakutanisha na masoko, kuwapa mafunzo pamoja na kuwapeleka kwenye fursa mbalimbali zilizopo ndani na nje ya nchi,ili kukuza biashara zao,kuchangia pato la taifa na kutoa ajira kwa vijana na wengine.

Kwa upande wake Meneja wa  SIDO  Bakari Songwe alisema, kampeni hiyo ni  moja ya jitihada ya za shirika lao kuwasaidia wajasiriamali kwa kuhamasisha katika kuendeleza viwanda vidogo pamoja  kurasimisha bidhaa zao na ubora, ikiwa ni njia ya kumuunga mkono Rais ya kufikia uchumi wa  kati kupitia viwanda.

Naye Makamu Mwenyekiti wa  TCCIA Leopard Lema alisema,wajasiriamali wanatakiwa kufanya kazi kwa bidii,kufuata taratibu za serikali pamoja na kuhudhuria mafunzo na fursa mbalimbali ikiwemo hiyo ya amsha kiwanda,ili waweze kufanikiwa kwani yeye amefanikiwa kutokana na kupatiwa mafunzo na SIDO.

Hata hivyo Mwenyekiti wa TWCC Mwanza Mariam Munanka alisema, wanatoa elimu  kwa wamama wajasiriamali  na kuwawezesha kwenda kwenye maonyesho mbalimbali ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kupanua wigo wa  biashara, kuweza kujitambua na kuzalisha bidhaa bora.

Aidha Katibu wa Jukwaa la Wanawake Mwanza Grace Bunyinyiga alisema, hiyo ni fursa kwa wanawake mkoani hapa,hivyo wanatakiwa kuunda vikundi kwa ajili ya kuanzisha  viwanda vidogo,kwani maendeleo ya Mwanza yanaletwa na wao.

Vilevile mmoja wa  washiriki katika kampeni hiyo ambaye ni  mjasiriamali wa  kusindika asali Mariam  Nyanza alisema, ni  vema mwanamke kujitambua na kufanya kazi ili kuepuka  kuwa tegemezi kwa kuchangamkia fursa za kiuchumi na biashara zinazotolewa na mashirika mbalimbali.
Mwenyekiti wa TWCC Mwanza, Mariam Munanka akizungumza katika uzinduzi wa kampeni hiyo.
Meneja wa SIDO, Bakari Songwe akizungumza katika uzinduzi
Baadhi ya washiriki wa waliohudhuria uzinduzi huo.

No comments:

Powered by Blogger.