LIVE STREAM ADS

Header Ads

Mbunge Ilemela awataka wananchi kuwafichua wauguzi wasio waadilifu

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Judith  Ferdinand, BMG
Wananchi  wilayani Ilemela wametakiwa kutoa taarifa za wauguzi wa vituo vya afya vya serikali ambao siyo waadilifu wanaowatoza fedha za matibabu watoto chini ya umri wa miaka mitano  na wazee kuanzia miaka 60.

Wito huo ulitolewa jana na mbunge wa jimbo la Ilemela Dkt.Angeline Mabula wakati akizungumza na wananchi  wa Kata ya Shibula kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika shule ya msingi Monze.

Dkt.Mabula ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi alisema serikali  imeweka utaratibu  wa matibabu  kwa watoto chini  ya umri wa miaka mitano, wamama wajawazito na wazee wenye miaka kuanzia 60 kupata huduma za afya bure katika vituo vyote  vya afya vya serikali hivyo wananchi wanatakiwa kutoa taarifa za baadhi  ya wauguzi ambao siyo waadilifu  na wanaoenda kinyume na taratibu kwa kuwatoza fedha.

"Kumekuwa na malalamiko juu ya baadhi ya wauguzi wa afya kuwatoza fedha za matibabu watoto wenye umri chini ya miaka mitano na wazee wenye miaka kuanzia 60, nawaomba mtoe taarifa  ili hatua kali dhidi yao zitachukuliwe huku  na nyie mkitimiza wajibu wenu kwa kupeleka watoto kliniki. Alisema Dkt. Mabula.

Kwa upande  wake diwani wa Kata ya Shibula, Dede Swila aliwahimiza wananchi kutimiza wajibu wao wa kuwapeleka watoto kliniki huku akina mama wajawazito nao wakiwa na utamaduni kwa kuhudhuria kliniki.

Awali baadhi ya wananchi wa Kata ya Shibula walitoa malalamiko  wa mbunge wao kuhusu baadhi ya wauguzi katika vituo vya afya kuwatoza fedha pale wanaposhindwa kuhudhuria kliniki kuanzia muda wa mwezi moja.

No comments:

Powered by Blogger.