LIVE STREAM ADS

Header Ads

Maadhimisho ya Nane Nane 2018 kitaifa yafunguliwa rasmi Bariadi mkoani Simiyu

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Mgeni rasmi-Waziri wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza kwenye sherehe za maadhimisho ya 25 ya Nanenane kwa mwaka 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi, Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu jana tarehe 3 Agosti 2018.

 Na Mathias Canal, WK-Simiyu
Waziri wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba, jana 3 Agosti 2018 amezindua maadhimisho ya 25 ya Nanenane kwa mwaka 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi, Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu huku akitoa wito kwa wananchi wote wa mikoa  inayounda kanda ya Ziwa Mashariki ambayo inayojumuisha mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga kutumia fursa ya kutembelea katika maonesho hayo ili kujifunza mbinu mbalimbali za kitaalamu katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi.

Akizungumza na mamia ya wananchi waliojitokeza kwenye uzinduzi wa maonesho hayo Dkt Tizeba aliwasihi wananchi wote kutumia fursa ya maonesho hayo kwa kuwatumia ipasavyo wataalamu ambao watakuwepo katika viwanja hivyo kwa siku zote za maonesho hayo ili kupata ushauri na maelekezo ya kuboresha shughuli zao za kiuchumi kupitia Kilimo, Ufugaji, Uvuvi na Ushirika.

Alisema kuwa wananchi wanapaswa kutembelea katika maonesho hayo kwa lengo la kujifunza ili kuwa tayari kuanza kutumia teknolojia na maarifa watakayopata kwa lengo la kujiletea mapinduzi halisi katika kilimo, mifugo na uvuvi.

Mhe waziri Tizeba alisema kuwa sekta ya kilimo nchini itaendelea kuwa sekta muhimu katika maendeleo ya uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla hususani katika wakati huu ambapo serikali imejidhatiti kufikia uchumi wa viwanda. Alisema sekta ya kilimo imeendelea kuimarika kwa kuchangia Pato la Taifa hadi asilimia 30.1 kwa mwaka 2017 ikilinganishwa na asilimia 29.2 mwaka 2016.

Sambamba na hayo Mhe Tizeba alisema kuwa ushirika ni sekta mtambuka inayohusisha sekta mbalimbali zikiwemo Kilimo, Ufugaji, Uvuvi, Madini, Viwand, Nyumba na Fedha (Ushirika wa Akiba, Mikopo na Benki) ambazo zinagusa wananchi wengi zaidi.

Alisema kutokana na umuhimu wa sekta hiyo, Wizara kupitia Tume ya maendeleo ya ushirika imeendelea kuwezesha na kuimarisha ushirika ili wananchi waweze kunufaika na fursa zinazopatikana katika ushirika kwa lengo la kuchangia katika kuongeza kipato kwa wananchi wengi hususani waliopo vijijini.
Alisema katika mwaka 2017/2018, Tume imefanya uhamasishaji wa wananchi kujiunga au kuanzisha vyama vya ushirika ambapo hadi kufikia Disemba 2017 vyama vipya 394 vilisajiliwa na kufanya idadi ya vyama vya ushirika kufikia 10,990 kutoka 10,596 vilivyokuwepo Machi 2017.

Alisema vyama hivyo vinakadiriwa kutoa ajira mpya kwa wananchi takribani 1,182 huku katika kipindi cha mwaka 2017/2018 wanachama wapya 385,295 walijiunga au kuanzisha vyama vya ushirika na kufanya idadi ya wanachama kuongezeka kutoka 2,234,016 hadi kufikia 2,619,311.

Kilele cha maadhimisho ya 25 ya Nanenane kwa mwaka 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi, Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu ni Tarehe 8 Agosti 2018 ambapo Rais Mstaafu wa awamu ya tatu nchini Tanzania Mhe Benjamin Willium Mkapa atakuwa mgeni rasmi akimuwakilisha Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.
Waziri wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba akisisitiza kilimo cha vitunguu vidogo ambavyo soko lake ni kubwa kuliko vitunguu vidogo mara baada ya kutembelea Banda la Jeshi la Kujenga Taifa (JKT)
Mgeni rasmi-Waziri wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba, Mhe Antony Mtaka Mkuu wa Mkoa mwenyeji wa sherehe za maadhimisho ya Nanenane kwa mwaka 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi, Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu
Mgeni rasmi-Waziri wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba akisisitiza jambo wakati akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza kwenye sherehe za maadhimisho ya 25 ya Nanenane kwa mwaka 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi, Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu
Mgeni rasmi-Waziri wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba akipiga ngoma ya asili ya kabila la kisukuma ishara ya uzinduzi wa sherehe za maadhimisho ya 25 ya Nanenane Kitaifa kwa mwaka 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi, Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu jana tarehe 3 Agosti 2018.

Wengine pichani (Kulia) ni Katibu Mkuu wizara ya mifugo na Uvuvi Prof Elisante Ole Gabriel, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe Adam Malima, Ndg Enock Yakobo na Kushoto ni Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu Ndg Jumanne Sagini, Naibu waziri wa kilimo Mhe Dkt Mary Mwanjelwa, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka na Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe Abdallah Ulega.

No comments:

Powered by Blogger.