Maadhimisho ya Nane Nane 2018 kitaifa yafunguliwa rasmi Bariadi mkoani Simiyu
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Na Mathias
Canal, WK-Simiyu
Mgeni rasmi-Waziri wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba
akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza kwenye sherehe za maadhimisho ya 25
ya Nanenane kwa mwaka 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi, Halmashauri ya Wilaya
ya Bariadi Mkoani Simiyu jana tarehe 3 Agosti 2018.
Waziri wa
kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba, jana 3 Agosti 2018 amezindua maadhimisho ya 25
ya Nanenane kwa mwaka 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi, Halmashauri ya Wilaya
ya Bariadi Mkoani Simiyu huku akitoa wito kwa wananchi wote wa mikoa inayounda kanda ya Ziwa Mashariki ambayo
inayojumuisha mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga kutumia fursa ya kutembelea
katika maonesho hayo ili kujifunza mbinu mbalimbali za kitaalamu katika sekta
za kilimo, mifugo na uvuvi.
Akizungumza
na mamia ya wananchi waliojitokeza kwenye uzinduzi wa maonesho hayo Dkt Tizeba
aliwasihi wananchi wote kutumia fursa ya maonesho hayo kwa kuwatumia ipasavyo
wataalamu ambao watakuwepo katika viwanja hivyo kwa siku zote za maonesho hayo
ili kupata ushauri na maelekezo ya kuboresha shughuli zao za kiuchumi kupitia
Kilimo, Ufugaji, Uvuvi na Ushirika.
Alisema kuwa
wananchi wanapaswa kutembelea katika maonesho hayo kwa lengo la kujifunza ili
kuwa tayari kuanza kutumia teknolojia na maarifa watakayopata kwa lengo la
kujiletea mapinduzi halisi katika kilimo, mifugo na uvuvi.
Mhe waziri
Tizeba alisema kuwa sekta ya kilimo nchini itaendelea kuwa sekta muhimu katika
maendeleo ya uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla hususani katika wakati huu
ambapo serikali imejidhatiti kufikia uchumi wa viwanda. Alisema sekta ya kilimo
imeendelea kuimarika kwa kuchangia Pato la Taifa hadi asilimia 30.1 kwa mwaka
2017 ikilinganishwa na asilimia 29.2 mwaka 2016.
Sambamba na
hayo Mhe Tizeba alisema kuwa ushirika ni sekta mtambuka inayohusisha sekta
mbalimbali zikiwemo Kilimo, Ufugaji, Uvuvi, Madini, Viwand, Nyumba na Fedha
(Ushirika wa Akiba, Mikopo na Benki) ambazo zinagusa wananchi wengi zaidi.
Alisema
kutokana na umuhimu wa sekta hiyo, Wizara kupitia Tume ya maendeleo ya ushirika
imeendelea kuwezesha na kuimarisha ushirika ili wananchi waweze kunufaika na
fursa zinazopatikana katika ushirika kwa lengo la kuchangia katika kuongeza
kipato kwa wananchi wengi hususani waliopo vijijini.
Alisema
katika mwaka 2017/2018, Tume imefanya uhamasishaji wa wananchi kujiunga au
kuanzisha vyama vya ushirika ambapo hadi kufikia Disemba 2017 vyama vipya 394
vilisajiliwa na kufanya idadi ya vyama vya ushirika kufikia 10,990 kutoka
10,596 vilivyokuwepo Machi 2017.
Alisema
vyama hivyo vinakadiriwa kutoa ajira mpya kwa wananchi takribani 1,182 huku
katika kipindi cha mwaka 2017/2018 wanachama wapya 385,295 walijiunga au
kuanzisha vyama vya ushirika na kufanya idadi ya wanachama kuongezeka kutoka
2,234,016 hadi kufikia 2,619,311.
Kilele cha
maadhimisho ya 25 ya Nanenane kwa mwaka 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi,
Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu ni Tarehe 8 Agosti 2018 ambapo
Rais Mstaafu wa awamu ya tatu nchini Tanzania Mhe Benjamin Willium Mkapa
atakuwa mgeni rasmi akimuwakilisha Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dkt John Pombe Magufuli.
Waziri wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba akisisitiza kilimo
cha vitunguu vidogo ambavyo soko lake ni kubwa kuliko vitunguu vidogo mara
baada ya kutembelea Banda la Jeshi la Kujenga Taifa (JKT)
Mgeni rasmi-Waziri wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba, Mhe
Antony Mtaka Mkuu wa Mkoa mwenyeji wa sherehe za maadhimisho ya Nanenane kwa
mwaka 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi, Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
Mkoani Simiyu
Mgeni rasmi-Waziri wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba
akisisitiza jambo wakati akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza kwenye
sherehe za maadhimisho ya 25 ya Nanenane kwa mwaka 2018 katika Viwanja vya
Nyakabindi, Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu
Mgeni
rasmi-Waziri wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba akipiga ngoma ya asili ya kabila
la kisukuma ishara ya uzinduzi wa sherehe za maadhimisho ya 25 ya Nanenane
Kitaifa kwa mwaka 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi, Halmashauri ya Wilaya ya
Bariadi Mkoani Simiyu jana tarehe 3 Agosti 2018.
Wengine
pichani (Kulia) ni Katibu Mkuu wizara ya mifugo na Uvuvi Prof Elisante Ole
Gabriel, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe Adam Malima, Ndg Enock Yakobo na Kushoto ni
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu Ndg Jumanne Sagini, Naibu waziri wa kilimo Mhe Dkt
Mary Mwanjelwa, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka na Naibu waziri wa
Mifugo na Uvuvi Mhe Abdallah Ulega.
No comments: