Mbunge wa Bukombe azindua wodi ya kisasa ya Mama na Mtoto
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mbunge wa
Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Mashaka Biteko (CCM) amezindua rasmi wodi
ya akina mama na watoto katika Kituo cha Afya cha Charles Kulwa Memorial
kilichopo Runzewe jimboni humo.
Biteko
ambaye pia ni Naibu Waziri wa Madini amefanya uzinduzi huo jana Agosti 08, 2018
alipofika katika Kata ya Uyovu kuzungumza na wananchi wa Kata hiyo kupitia
mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Kabulima.
Akizungumza
kwenye uzinduzi huo, Biteko aliupongeza uongozi wa kituo hicho cha binafsi kwa
kujenga wodi hiyo yenye vifaa vya kisasa na kutoa rai kuwahudumia wananchi wote
kwa kuzingatia taratibu zote za afya ikiwemo kutowabagua wanaotumia bima ya
afya.
Mkurugenzi
wa kito hicho, Dkt.Baraka Kulwa alisema kilianza kama Zahanati mwaka 1997 kabla
ya kupandishwa hadhi mwaka 2015 na kuwa Kituo cha Afya ambapo kinahudumia
wagonjwa kati ya 3,000 hadi 4,000 kwa mwezi huku asilimia zaidi ya 70 wakiwa ni
akina mama na watoto hivyo ujenzi wa wodi hiyo iliyogarimu takribani shilingi
milioni 25 utasaidia kuboresha zaidi huduma za afya kituoni hapo.
“Kwa kweli nashukuru
kwa uzinduzi wa huduma hii, inatusaidia sana. Mimi natoka Kakonko lakini
nimekuwa nikisikia kwamba hapa kuna huduma nzuri”. Alisema mama Winfrida John
ambaye ni mkazi wa Kakonko aliyefika kituoni hapo kwa ajili ya kupata huduma.
No comments: